Page 66 - Fasihi_Kisw_F5
P. 66

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              riwaya ya Njama, (Musiba 1986), Tete na Mwadi kwenye riwaya ya Kikosi cha
              Kisasi, (Musiba 2018), pamoja na Nyaso kwenye riwaya ya Hofu (Musiba 2018).

              (vii) Huiga mawazo na matendo ya filamu za kigeni
          FOR ONLINE READING ONLY
              Riwaya pendwa nyingi za Kiswahili, hasa za miaka ya 1980, ni mwigo wa
              maandishi ya Kimagharibi pamoja na filamu za Kizungu na Kiasia zinazohusu
              upelelezi,  ujasusi, uhalifu na mapenzi.  Wasomaji wengi wameifanya riwaya
              pendwa  kama  kibadala  au  kijalizo  cha  filamu.  Kwa  mfano,  Musiba  kwenye
              riwaya  zake  amemchora  mhusika  mkuu, Willy  Gamba,  kwa  kumpa  ujuzi  wa
              kupigana kininja katika mapambano dhidi ya majasusi. Kupigana kwa kufuata
              sheria za kininja, mara nyingi, ni mbinu zinazotumiwa na filamu za Kimagharibi
              na Kimashariki.

               Shughuli 2.15
              Soma riwaya na hadithi fupi teule, kisha eleza tofauti ya tanzu hizo.


                                Zoezi la 2.3


                 1.   Kwa kutumia mifano, tofautisha dhana zifuatazo:

                     (a)  melodrama na ramsa
                     (b)  utao na ukwapi

                     (c)  riwaya za kihistoria na za sira

                     (d)  mashairi na tenzi
                     (e)  riwaya za kifalsafa na za kisaikolojia


                 2.   “Riwaya ni zao la fasihi simulizi.” Jadili
                 3.   “Tamthiliya za Kitanzania za sasa ni zao la tamthiliya za Kimagharibi.”
                     Jadili.

                 4.   Eleza  kwa  ufupi  namna  dhana  ya  utendaji  inavyojitokeza  katika
                     tamthiliya.

                 5.   Kwa kutumia mifano, eleza aina za tamthiliya na namna
                     zinavyotofautiana.
                 6.   Kwa kutumia mifano, jadili mabadiliko ya ushairi wa Kiswahili katika
                     vipindi mbalimbali.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            55
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   55                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   55
   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71