Page 63 - Fasihi_Kisw_F5
P. 63

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              mwa vifo hivyo ni kile cha mama yake Gusto, dada yake (Nandi) na mjomba
              wake Gusto (Kapedzile). Kuwapo kwa matukio mengi ya kichawi kunaleta hofu
              kwa wasomaji wa riwaya hii. Zaidi, matendo yanayotendeka wakati Gusto akila
              kiapo cha uchawi yanatisha mno.
          FOR ONLINE READING ONLY
              (o)  Riwaya za watoto na vijalunga
              Riwaya  za  watoto  na  vijalunga  hutofautiana  na  riwaya  za  watu  wazima  kwa
              sifa kadhaa, zikiwamo za aina za wahusika, muundo, msuko, uchache wa visa,
              michoro na picha, matumizi ya fantasia na fonti zinazotumika. Vilevile, riwaya za
              watoto huepuka kusawiri matukio hasi kama vile ya mauaji, masuala ya ngono,
              na mahusiano ya jinsia moja. Mifano ya riwaya hizo ni Safari ya Prospa (Lema,
              1995),  Kimbia Helena Kimbia (Mnyaka, 1995),  Moto wa Mianzi (Mulokozi,
              1996) na Marimba ya Majaliwa (Semzaba, 2008).

              2.  Riwaya pendwa

              Riwaya pendwa ni zile ambazo hutumia fani inayojichomoza na kusisimua zaidi
              kiasi cha kuweza kufunika maudhui. Hali hii huifanya riwaya hizi zionekane kuwa
              na lengo la kustarehesha au kuburudisha wasomaji tu. Mambo yanayosawiriwa
              sana na waandishi wa riwaya za kundi hili ni mapenzi, upelelezi, ujasusi, ugaidi,
              ujambazi na mauaji. Waandishi wa riwaya pendwa huyasawiri mambo hayo kwa
              ufundi mkubwa; na hupangilia visa na vituko kwa namna inayosisimua. Nchini
              Tanzania, aina hii ya riwaya iliandikwa kwa mara ya kwanza na Muhamed Said
              Abdulla (MSA) alipoandika riwaya ya Mzimu wa Watu wa Kale (1957). Mifano
              mingine ya riwaya hizi ni Simu ya Kifo (Katalambula, 1965), Kisima cha Giningi
              (Abdulla, 1968) na  Njama  (Musiba, 1981). Uandishi wa riwaya za aina hii
              uliongezeka maradufu katika miaka ya 1980, kutokana na matatizo ya kiuchumi.

              Sifa za riwaya pendwa
              Riwaya pendwa zina sifa zifuatazo:

              (i)  Hutumia taharuki kwa kiasi kikubwa

              Taharuki  ni hamu  kubwa anayokuwa nayo msomaji  kutaka  kujua  mambo
              yatakayotokea na yatakavyotokea katika hadithi. Taharuki hutumiwa kwa kiasi
              kikubwa katika riwaya pendwa kupitia matukio ya kusisimua yanayojibainisha
              kupitia migogoro iliyosukwa kwa ufundi. Taharuki inafikia kilele wakati fumbo
              linapofumbuliwa  kwa kujibiwa maswali  kadhaa  yaliyojitokeza  akilini  mwa
              msomaji. Kwa mfano, katika riwaya ya Mzimu wa Watu wa Kale (Abdulla, 1957)
              swali linalojitokeza ni: nani amemuua Bwana Ali Bomani? Mbinu za awali za




                52                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   52                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   52
   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67   68