Page 58 - Fasihi_Kisw_F5
P. 58

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kazi zilizosawiri maisha yaliyopita. Mfano wa riwaya za kundi hili ni Mtu ni Utu
              (Mhina, 1971) na Njozi za Usiku (Seme, 1976). Kundi la pili ni lile lililouona
              ujamaa kwa jicho la matarajio kwamba kuna ujenzi wa jamii mpya itakayoishi
              vizuri kuliko jamii iliyokuwapo. Kwa hiyo, kundi hili liliandika kazi kwa shauku
          FOR ONLINE READING ONLY
              ya kueleza mabadiliko yatakayoletwa na vijiji vya ujamaa. Mfano wa riwaya
              hizo ni Shida (Balisidya, 1975) na Ndoto ya Ndaria (Ngomoi, 1976). Riwaya
              hizi zililenga kuonesha ubora wa maisha ya vijijini. Muundo wa riwaya hizi ni
              wa moja kwa moja, lugha nyepesi na wahusika wasio na utata.

              Pia, katika kipindi hiki, walijitokeza waandishi walioandika riwaya kwa jicho
              la kiyakinifu. Riwaya za namna hii ziliyasawiri masuala ya kijamii kipembuzi.
              Mifano ya riwaya hizo ni Kasri ya Mwinyi Fuad (Shafi, 1978), Kuli (Shafi, 1979)
              na Dunia Mti Mkavu (Mohamed, 1979). Waandishi wa riwaya hizi wanaeleza
              mapambano dhidi ya umwinyi na ubepari. Katika riwaya ya Kasri ya Mwinyi
              Fuad, kwa mfano, kuna mvutano baina ya mamwinyi, watwana na watumwa.
              Pande hizi mbili zinakinzana na hatimaye, mikinzano inazaa mapinduzi. Kwa
              kiasi, waandishi hawa waliathiriwa na fikra za Ki-Marx (Senkoro, 1984).


              Katika miaka ya 1980, liliibuka wimbi la uandishi wa riwaya pendwa. Riwaya
              hizi zilizuka kutokana na sababu za kiuchumi, ambapo uchumi wa  Tanzania
              uliyumba  kutokana  na  Vita  vya Kagera, majanga  kama  ukame,  pamoja  na
              masharti magumu ya Shirika la Fedha la Kimataifa na Benki ya Dunia. Waandishi
              wengi walianza kuandika riwaya pendwa kwa lengo la kujipatia fedha za haraka.
              Pia, zilizuka kampuni nyingi za uchapishaji nchini. Kampuni hizo zilirahisisha
              uchapishaji  wa riwaya pendwa kwa haraka na kwa gharama nafuu. Soko la
              riwaya pendwa lilikuwa kubwa kutokana na maudhui yake kupendwa na watu
              wa rika zote. Aidha, waandishi ndio walikuwa wachapishaji na wauzaji wakuu
              wa riwaya hizo. Miongoni mwa riwaya hizo ni Tutarudi na Roho Zetu (Mtobwa
              1987), Roho Mkononi (Rajab,1984), Dimbwi la Damu (Mtobwa, 1984), Kikomo
              (Musiba,  1980)  na  Njama  (Musiba,  1981).  Nyingine  ni  Kijasho  Chembamba
              (Ganzel, 1980), Ufunguo wa Bandia (Rajab, 1974), Jeraha la Moyo (Kiango,
              1974) na Kwa Sababu ya Fedha (Simbamwene, 1972).

              Pia, katika  kipindi  hiki  waandishi  wengi waliandika  riwaya  zilizohakiki
              jamii.  Riwaya hizi  zilitokana  na Azimio  la Arusha kutokukidhi  matarajio  ya
              Watanzania.  Wasanii  waliandika  riwaya  kueleza  maoni  yao kuhusu viongozi
              walioaminika  kuwaongoza  wananchi  kuyafikia  malengo  ya  vijiji  vya  ujamaa.
              Viongozi waligeuka wasaliti, waroho, na wazembe huku wakiendekeza rushwa,
              uvivu, ulevi na ubadhirifu wa mali ya umma. Mfano wa riwaya za kipindi hicho



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            47
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   47                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   47
   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62   63