Page 54 - Fasihi_Kisw_F5
P. 54

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Tofauti baina ya michezo ya fasihi simulizi na tamthiliya za fasihi andishi
              Michezo  ya fasihi simulizi hutofautiana  na tamthiliya za fasihi andishi kwa
              vipengele vifuatavyo:


              (a)  Utunzi wa maonesho
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mara nyingi mtungaji  wa mchezo  na mwigizaji  wa tamthiliya  huwa tofauti.
              Maneno ya mtunzi  ni lazima  yakaririwe  na waigizaji  jinsi  yalivyo  au kama
              madokezo  ya  lazima.  Kwa upande  wa fasihi  simulizi,  mara  kadhaa  watunzi
              wa mchezo  ndio wachezaji.  Maneno na vitendo  ni vyao wenyewe na wakati
              mwingine hubuniwa papo kwa papo.

              (b)  Maandalizi
              Tamthiliya hupitia maandalizi kadhaa kama vile kufanya mazoezi mengi kabla ya
              kuigizwa jukwaani. Pia, jukwaa na vyombo vitakavyotumika sharti viandaliwe
              mapema. Kwa ujumla, igizo lolote ili livutie watazamaji linapaswa kufanyiwa
              maandalizi mazuri. Kwa upande wa maandalizi drama zinazotokana na vitabu na
              zile zinazotungwa tu kichwani lazima ziandaliwe vizuri.

              (c)  Shabaha
              Shabaha kuu katika drama na maigizo ya kawaida ni kuelimisha, kuburudisha na
              wakati mwingine ni biashara kwa sababu watu hununua tamthiliya au huuza kazi
              hizo katika vituo vya runinga na redio. Vilevile, maigizo huoneshwa ukumbini
              ambapo watazamaji hupaswa kulipia.

               Shughuli 2.13
              Kwa kutumia vyanzo vya maktabani,  soma tamthiliya  mbili  au zaidi,  kisha
              bainisha aina ya tamthiliya hizo.

               Shughuli 2.14
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, jadili dhana na aina za riwaya.


              Riwaya
              Riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni itumiayo lugha ya kinathari (lugha ya mjazo)
              yenye  uchangamani  wa  visa,  wahusika,  mandhari  na  dhamira.  Mara  nyingi
              vipengele  hivyo huakisi  maisha  ya jamii  inayohusika.  Hivyo, riwaya  huweza
              kutoa  picha  ya  jumla  ya  maisha  ya  mtu  kutoka  nyumbani  (mtu  binafsi)  hadi
              kiwango cha taifa na hata dunia nzima (Mohamed, 1995; Madumulla, 2009; na
              Senkoro, 2011).






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            43
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   43                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   43
   49   50   51   52   53   54   55   56   57   58   59