Page 52 - Fasihi_Kisw_F5
P. 52

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              1969), Mashetani (Hussein, 1971), Hatia (Muhando, 1972), Tambueni Haki Zetu
              (Muhando, 1973), Aliyeonja Pepo (Topan, 1973) na Pambo (Muhando, 1975).
              Nyingine ni Sundiata (Mbogo, 1975), Jogoo Kijijini na Ngao ya Jadi (Hussein,
              1976), Machozi ya Mwanamke (Ngozi, 1977), Mukwava wa Uhehe (Mulokozi,
          FOR ONLINE READING ONLY
              1979), Arusi (Hussein, 1980), Tendehogo (Semzaba, 1984), na Giza Limeingia
              (Mbogo, 1980). Vilevile,  kulikuwa na  Njia Panda  (Muhanika, 1981)  Tone la
              Mwisho (Mbogo, 1981), Nguzo Mama (Muhando, 1982), Lina Ubani (Muhando,
              1984), Kwenye Ukingo wa Thim (Hussein, 1988), Pungwa (Mohamed 1988),
              Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe (Semzaba, 1988) Kivuli Kinaishi (Mohamed
              1990), na Morani (Mbogo, 1993).

              Tamthiliya zimeendelea kutungwa zikiakisi mabadiliko ya mifumo ya maisha
              ya jamii  ya wakati  huo. Mathalani,  tamthiliya  kama  Ushuhuda wa Mifupa
              (Ngozi, 1990) na Kilio Chetu (Medical Aid Foundation, 1995) zimejadili kuhusu
              maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI katika jamii.


              Miaka ya karibuni, tamthiliya ya kihistoria imeanza kushamiri tena baada ya
              kupotea  kwa takribani  miongo mitatu  tangu  enzi  za  Kinjekitile  na  Mukwava
              wa Uhehe. Mtunzi  aliyejipambanua  zaidi  katika  mkondo huu ni Emmanuel
              Mbogo ambaye ametoa tamthiliya nne katika miaka ya karibuni. Tamthiliya hizi
              zinaongeza idadi ya tamthiliya zake nyingine mbili za kihistoria alizozichapisha
              hapo kabla. Nazo ni Ngoma ya Ng’wanamalundi (1988), Sundiata (1994), Fumo
              Lyongo (2009), Sadaka ya John Okello (2015), Nyerere na Safari ya Kanaani
              (2015), Malkia Bibi Titi Mohamed (2016) na Shujaa Mirambo (2021). Tamthiliya
              hizo, mbali na kupevua mkondo wa tamthiliya  ya kihistoria,  zinadhihirisha
              namna  historia  inavyoweza  kutumika  kisanaa  kusawiri  migogoro  na  masuala
              yenye umuhimu katika jamii ya leo.

              Aina za tamthiliya
              Tunaweza kuainisha tamthiliya kwa kutumia vigezo mbalimbali kama vile kigezo
              cha maudhui, kusudio, dhima, muktadha wa utendaji, hadhira lengwa na mbinu
              za kisanii. Kila kigezo hutupatia aina mahususi za tamthiliya. Mathalani, kigezo
              cha hadhira lengwa kinapotumika, huweza kutupatia aina zifuatazo: tamthiliya ya
              watoto, tamthiliya ya vijana, tamthiliya ya watu wazima, tamthiliya ya wanawake,
              tamthiliya ya wanaume, tamthiliya ya miungu na tamthiliya ya waumini wa dini
              fulani. Uainishaji uliotumika katika kitabu hiki umetumia kigezo cha mbinu za
              kisanaa. Kwa kuzingatia kigezo hicho, tunapata aina zifuatazo: tanzia, ramsa,
              tanzia ramsa, na melodrama.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            41
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   41                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   41
   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56   57