Page 48 - Fasihi_Kisw_F5
P. 48

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                  3.  Majonzi hayaneneki, kila nikikumbukia,

                     Nawaza kile na hiki, naona kama ruia,

                     Mauti sijasadiki, kuwa mwisho wa dunia,
          FOR ONLINE READING ONLY
                     Mapenzi tuliyofunga, hapana wa kufungua.


              Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini (Robert, 2003:5)

              Maswali
                   (a)  Andika ujumbe wa shairi.

                   (b)  Bainisha mloto wa ubeti wa pili.

                   (c)  Bainisha vina vya kati na vya mwisho vya ubeti wa pili.
                   (d)  Orodhesha utao wa ubeti wa kwanza na ukwapi wa ubeti wa tatu.
                   (e)  Orodhesha mizani ya uketo wa kibwagizo cha shairi hili.



               Shughuli ya 2.10

              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, jadili dhana na historia ya
              hadithi fupi ya Kiswahili.

              Hadithi fupi
              Hadithi fupi ni simulizi za kubuni zinazosawiri tukio, tabia, mgogoro au kipengele
              cha maisha kwa ufupi. Hadithi za namna hii huwa na tukio moja au mawili na
              hutumia mawanda finyu. Kwa kawaida, hadithi fupi haina uchangamano mkubwa
              wa matukio, na hutumia wahusika wachache.

              Historia ya hadithi fupi
              Chimbuko la utanzu wa hadithi fupi ni hadithi simulizi na andishi zinazopatikana
              katika lugha nyingi duniani. Baadhi ya fani zilizochangia kuchipuka kwa hadithi
              fupi ni ngano, hekaya, visa, michapo na tendi. Kuzuka kwa fani ya hadithi fupi
              huko Marekani na Ulaya katika karne ya 19 kulisaidiwa sana na kuchipuka kwa
              utamaduni wa kusoma magazeti, kwani visa vingi vilichapishwa katika magazeti
              hayo. Uhusiano huu kati ya hadithi fupi na magazeti au majarida bado upo hadi
              leo.

              Historia ya hadithi fupi haitofautiani sana na historia ya riwaya ya Kiswahili.
              Visa vya mwanzo vilivyochapishwa kwa Kiswahili ni mkusanyiko wa hekaya
              na ngano. Baadhi ya hadithi hizo ni zile zinazopatikana katika vitabu vifuatavyo:


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            37
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   37                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   37
   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53