Page 45 - Fasihi_Kisw_F5
P. 45

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                               MDADISI
                               Ni mafunzo yapi hayo, ya hekima na ubora?

                               Yatiayo wangu moyo, kwa jitihada na ghera,
          FOR ONLINE READING ONLY
                               Ufanisi yaletayo, ya kugeuza majira,

                               Maana yake ngonjera, nambie nami nijue.

                               JAWABU

                               Mafunzo yatolewayo, kwa usemi wa hadhara,
                               Mema yachangamshayo, kwa tabasamu ya sura,

                               Ni ghibu itumikayo, kwa fikira na busara,

                               Maana yake ngonjera, ni mafunzo kwa shairi.


                               Ngonjera za Ukuta: Kitabu cha Kwanza (Mnyampala, 1970:5)

              (iii)  Ushairi wa kidrama
              Huu ni ushairi unaotumiwa katika baadhi ya tamthiliya kama mtindo mmojawapo
              wa kuandika mazungumzo ya wahusika. Hivyo, hauwezi kutenganishwa na fani
              ya tamthiliya (Mulokozi, 2017). Ufuatao ni mfano wa ushairi huu:


                               Mwanamke
                               Ndugu zangu, pulikeni ndugu zangu

                               Sasa si kama zamani

                               Sasa umetawala uwazi

                               Uwazi na utambuzi

                               Tusipigwe na bumbuwazi

                               Tusijisabilie kirahisi

                               Kwa ndoa yenye wasiwasi!
                               Mume mwenyewe kumwakisi

                               Bali hukufanya kisisi

                               Ukanipa mchumba mwenye ukakasi…




                34                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   34                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   34
   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50