Page 41 - Fasihi_Kisw_F5
P. 41

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Vipera vya ushairi andishi
              Ushairi andishi umegawanyika katika vipera vitatu. Vipera hivyo ni mashairi,
              tenzi na ushairi wa maigizo.


              (a)  Mashairi
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kuna mitazamo miwili inayohusu mashairi: mtazamo wa kimapokeo na mtazamo
              wa kisasa.
              Mtazamo wa kimapokeo
              Huu ndio mtazamo wa awali kuhusu mashairi ya Kiswahili. Wafuasi wa mtazamo
              huu wanasisitiza mambo yafuatayo: kanuni za urari wa vina na mizani, na lugha
              nzito ya mkato. Urari wa vina na mizani hulifanya shairi liimbike kwa urahisi
              kwa mahadhi yanayofahamika. Tazama mfano wa beti zifuatazo:



                              Maisha
                              Maisha kitendawili, kitegue kwa busara,

                              Uitulize akili, huku ukiwa tohara,

                              Uhimili kila hali, yaweza kwako kung’ara,

                              Tukiimudu subira, maisha hayatuwengi.



                              Maisha kama bahari, yenda mpera mpera,
                              Vyovyote uwe tayari, kwa kujiweka imara,

                              Na kumuomba Kahari, akunyooshee dira,
                              Tukiimudu subira, maisha hayatuwengi.




                              Maisha ni kujituma, ili uipate tira,

                              Ushughulike kulima, au kuunda minara,
                              Mwiko kujiweka nyuma, utakumbwa na idhara,

                              Tukiimudu subira, maisha hayatuwengi.



                              Diwani ya Tunzo ya Ushairi ya Ebrahim Hussein (Juma (Mwana

                            wa Nyasa), 2016).


                30                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   30
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   30                    23/06/2024   17:54
   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46