Page 42 - Fasihi_Kisw_F5
P. 42

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Shairi hili lina mizani linganifu. Kila mshororo una mizani kumi na sita na vina
              vinavyofanana  mwishoni mwa kila  mshororo kwa shairi zima. Vina  vya kati
              vinafanana katika kila ubeti. Kila ubeti umeundwa na mistari minne, ambapo
              huu ni muundo wa tarbia.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mtazamo wa kisasa au masivina
              Huu ni mtazamo wa wanamabadiliko wanaodai kwamba si lazima shairi liwe
              na urari wa vina wala ulinganifu wa mizani. Mtazamo huu ulianza mwishoni
              mwa miaka ya 1960 na kushadidiwa mwanzoni mwa miaka ya 1970. Wafuasi wa
              mtazamo huu ni Ebrahim Hussein, Euphrase Kezilahabi na Jared Angira. Wafuasi
              wengine ni Mugyabuso Mulokozi, Kulikoyela Kahigi, Said Ahmed Mohamed
              na Theobald Mvungi. Kulikoyela Kahigi na Mugyabuso Mulokozi wameandika
              Mashairi ya Kisasa (1973), Malenga wa Bara (1976) na Kunga za Ushairi na
              Diwani Yetu (1982), Said Ahmed Mohamed ameandika diwani kadhaa zikiwamo
              ‘Sikate Tamaa (1983) na Kina cha Maisha (1984).


              Wafuasi wa mtazamo huu wanaamini kuwa maudhui yanaweza kuwasilishwa
              bila kujikita  katika sheria za vina na mizani. Wanadai kuwa, kama ambavyo
              mabadiliko  yanatokea  katika  nyanja  nyingine,  ni lazima  pia  yatokee  katika
              ushairi.  Ikumbukwe kwamba,  wenye mtazamo  huu hawapingi  kanuni  za
              wanamapokeo, ila wamepanua wigo wa mashairi. Kwa mfano, zaidi ya nusu ya
              mashairi yaliyomo katika Diwani ya Malenga wa Bara (Kahigi na Mulokozi,
              1976) ni ya kimapokeo. Wanausasa wanatilia mkazo matumizi ya lugha kuliko
              muundo wa shairi. Tazama mfano wa shairi la kisasa la “Kuchambua Mchele”:


                               Habari zilifika kutoka Arusha,
                               Tukaanza kuchambua mchele wa Ujamaa,

                               Macho mbele, macho pembeni tukitoa mchanga,
                               Tukafanya kaburi dogo la mchanga.



                               Tukaanza kutoa chenga, moja moja,

                               Vidole vikafanya kazi kama cherehani,
                               Usiku na mchana; macho yakauma,

                               Tukafanya kichuguu kidogo cheupe.


                            Kichomi (Kezilahabi, 1988)



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            31
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   31                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   31
   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47