Page 38 - Fasihi_Kisw_F5
P. 38

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Baadhi ya sifa za maigizo ya watoto ni kuwa na muundo wa moja kwa moja na
              kutohitaji maleba mahususi.

               Shughuli ya 2.7
              Tumia vyanzo mbalimbali kuchunguza michezo mitatu ya watoto, kisha bainisha
          FOR ONLINE READING ONLY
              mbinu za kisanaa zilizotumika katika utunzi wa michezo hiyo.


                                Zoezi la 2.1


                 1.   Kwa kutumia mifano fasili dhana zifuatazo:
                     (a)   hurafa          (b)   soga            (c)  lakabu
                     (d)   istiara         (e)   visasuli        (f)   hekaya

                     (g)   ngomezi


                 2.   Kwa kutumia mifano, eleza tofauti kati ya ngano na vigano.

                 3.   Kwa kutumia mifano anuwai, tofautisha vichekesho na maigizo.

                 4.   Jadili athari za utani unaofanyika katika jamii yako.

                 5.   “Si kila mchezo wa watoto ni fasihi simulizi.” Jadili kauli hii kwa hoja
                     maridhawa.

                 6.   Kwa kutumia mifano, tofautisha dhana zifuatazo:

                     (a)  tendi na tenzi
                     (b)  maghani na nyimbo

                     (c)  visasili na visakale

                     (d)  vitendawili na mizungu

                     (e)  visasili na visasuli

                 7.   Chambua  mbinu za kisanaa  zinazojitokeza  katika  ngano, visasili,  na
                     soga.

                 8.   Sikiliza  ngano mbili  kutoka kwa wenzako  kisha  andika  insha  fupi
                     kueleza mafunzo yaliyomo katika ngano hizo.







                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            27
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   27                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   27
   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42   43