Page 37 - Fasihi_Kisw_F5
P. 37

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Ta la la la la la
              Kiota


              Wimbo wa mchezo huu huambatana na vitendo vya kutembea na kuzunguka.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Michezo mingi ya watoto hujumuisha pamoja nyimbo na vitendo.

              Maigizo ya watoto ni aina nyingine ya michezo ya watoto. Watoto huigiza michezo
              inayoakisi mazingira yanayowazunguka kama vile nyumbani, shuleni, shambani,
              hospitalini, barabarani, kanisani, msikitini na porini. Pia, watoto huigiza mambo
              wanayoyaona kwenye runinga, hasa watoto waishio mijini. Kwa mfano, huigiza
              michezo ya kivita, sherehe mbalimbali, vikundi vya nyimbo, miziki na michezo
              ya kuigiza.

              Maigizo ya watoto, kama ilivyo kwa kazi nyingine za fasihi, yana vipengele
              vya fani na maudhui. Maudhui ya michezo ya watoto, kwanza, huhusu maisha
              ya nyumbani kwa sababu ndiyo maisha wanayoyaona mara kwa mara. Watoto
              huigiza  maisha  ya nyumbani  kwa kuakisi  maisha  halisi  ya  familia,  hususani
              yale wanayoyaona kwenye kaya zao. Mathalani, kama baba au mama ni mkali,
              mtoto atakayewaigiza, ni lazima atakuwa mkali, pengine kuzidi ukali anaouona
              kwa wazazi wake; vivyo hivyo, kama baba au mama ni mpole na mkarimu basi
              muigizaji  ataigiza  upole na ukarimu  wao. Ikiwa mzazi  ni mchapakazi,  basi
              muigizaji atakuwa na tabia hiyo. Kama ni nadhifu, mwigizaji naye atajitahidi
              kuwa nadhifu. Kwa hiyo watoto waigizao nafasi ya wazazi wao, huakisi tabia ya
              wazazi hao.

              Kwa kawaida,  hakuna  matini  inayokuwa  imeandaliwa  kabla  ya  mchezo,  bali
              maigizo ya watoto hubuniwa papo kwa papo. Watoto wanapokutana hukubaliana
              aina  ya mchezo na kugawana  majukumu  ya kila  mhusika;  wakati  mwingine,
              watoto wenyewe huchagua nafasi watakazoigiza. Uigizaji wa michezo ya watoto
              huambatana na ubunifu ambapo kila mtoto (mhusika) hubuni uigizaji wa uhusika
              wake. Katika maigizo yanayohusisha wanyama, kwa mfano, kama igizo lina
              mhusika simba, mtoto anayeigiza kama simba ni lazima awe na sifa za ubabe,
              sauti nzito na nguvu. Halikadhalika, atakayeigiza kama jogoo, awe na sauti kali
              ili atakapowika asikike.

              Aidha, watoto huchagua nafasi kulingana na uwezo wao na jinsi jamii ilivyoainisha
              majukumu mbalimbali kama ya udaktari, ualimu, uaskari na mengineyo. Kwa
              hiyo, watoto huchagua nafasi za kuigiza kutokana na kazi wazipendazo. Wakati
              mwingine kupitia michezo hii, ndoto za watoto huchomoza na watoto wengine
              huanza kuishi na ndoto zao.


                26                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   26                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   26
   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42