Page 35 - Fasihi_Kisw_F5
P. 35

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Kama ilivyodokezwa katika maelezo  ya sanaa za maonesho kwa ujumla,
              vichekesho ni mojawapo ya sanaa mamboleo;  vichekesho vingi vimetokana
              na kuletwa kwa tamthiliya za kizungu zilizobeba na kuongelea utamaduni wa
              kimagharibi.  Baadhi  ziliongelea  matatizo  ya  kijamii  ya  wakati  wa ukoloni,
          FOR ONLINE READING ONLY
              mathalani suala la mgongano kati ya miji na vijiji, na uzuzu au ushamba wa
              Mwafrika anayetoka kijijini na kuingia mjini kwa mara ya kwanza. Maigizo hayo
              hayakuwa na maana kubwa kwa Waafrika zaidi ya kuwachekesha kupitia katika
              vitendo vilivyofanywa kwenye jukwaa. Kwa hiyo, Waafrika wakadhani kuwa
              jambo muhimu katika vichekesho ni kuchekesha.

              Kimsingi, dhima ya vichekesho si kuchekesha tu, bali vichekesho huelimisha pia.
              Mifano ya vichekesho ni kama ile inayopatikana katika vipindi vinavyorushwa na
              vituo vya redio, mitandao ya kijamii, na runinga. Mifano ya vipindi vya kwenye
              runinga ni Mizengwe (ITV), Futuhi (Star TV), Vitimbi Show (Channel Ten), na
              Kitimtim (DSTV).


              (d)  Ngomezi
              Hii ni sanaa ya kuwasiliana kupitia midundo ya ngoma. Baadhi ya jamii hupeana
              taarifa za matukio mbalimbali kupitia ngoma. Aghalabu, taarifa hizo huwa katika
              hali ya mafumbo, kiasi kwamba, wenyeji wa jamii husika tu huweza kubaini
              maana ya midundo husika. Hii yatokana na ukweli kuwa midundo katika sanaa
              hii hufuata kanuni maalumu zinazojulikana na wanajamii hao tu. Kanuni hizo
              hubebwa kupitia vipengele vya aina ya ngoma zinazotumika, muda wa kupigwa
              kwa ngoma pamoja na kasi au mwachano wa upigaji. Kanuni hizi huwasaidia
              wanajamii kupata ujumbe unaowasilishwa. Kwa mfano, katika jamii ya Wayao
              kuna ngoma inayojulikana  kama  Ngula-ntwe inayopigwa kwa ajili  ya kutoa
              ujumbe  kuhusu matukio  mbalimbali  ya kitanzia.  Kutokana  na mapigo  na
              midundo ya ngoma, ujumbe huo huweza kufasiliwa kuwa: “Simba amevamia
              na kuua mifugo”, “Simba amejeruhi mtu ila hajamuua”, “Simba ameua mtu”, au
              “Kesho wanaume wote wanatakiwa kwenda kwenye msako wa simba mvamizi.”


              (e)  Utani
              Ni hali ya kufanyiana mizaha au masihara baina ya watu ambapo hali hii ni tofauti
              na desturi za kutokuheshimiana.  Wanajamii  wenye uhusiano wa kutaniana,
              hutaniana mahali popote wakutanapo kama vile msibani, harusini, hata kwenye
              sehemu za kazi. Utani huweza kuwa kati ya mtu na mtu, ukoo na ukoo au kabila
              na kabila. Utani kati ya mtu na mtu huwa kati ya babu/bibi na wajukuu, mtu
              na shemeji au wifi na wifi. Kadhalika, utani kati ya kabila na kabila, aghalabu,
              huwa kati ya makabila yenye asili ya kuishi katika eneo moja au yaliyokuwa na



                24                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   24                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   24
   30   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40