Page 40 - Fasihi_Kisw_F5
P. 40

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kueleza maudhui yake kimuhtasari; na aghalabu, huyaficha maudhui hayo ndani
              ya taswira na ishara. Kama ilivyo kwa ushairi simulizi kwamba ndio utanzu wa
              kwanza kabisa wa fasihi simulizi, ushairi andishi nao ulikuwa utanzu wa kwanza
              wa fasihi andishi.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Historia fupi ya ushairi wa Kiswahili
              Tarehe mahususi za kuanza kwa ushairi wa Kiswahili, hususani umbo la ushairi
              linaloonekana  leo, ni za kukisia. Kilicho bayana ni kwamba, kabla ya karne
              ya 10 ushairi wa Waswahili ulikuwa ukitungwa na kughaniwa kwa ghibu bila
              kuandikwa.  Hali  ilibadilika  kuanzia  karne  ya  10 wakati  Uislamu  ulipoanza
              kuenea  Uswahilini;  na hivyo, kueneza  hati  ya Kiarabu. Kuanzia  wakati  huo,
              baadhi ya Waswahili walianza kutunga na kuandika mashairi, hasa tenzi na tendi,
              kwa kutumia hati hiyo.


              Wataalamu hugawa maendeleo ya ushairi wa Kiswahili katika mihula mbalimbali.
              Kwa mfano, Kezilahabi (1983) anabainisha mihula minne ambayo ni: muhula wa
              urasimi, muhula wa utasa, muhula wa urasimi mpya, na muhula wa sasa.

              Muhula wa Urasimi ni kipindi maalumu kinachochukuliwa kuwa msingi wa
              kuwekwa kwa sheria au kanuni ya jambo fulani. Urasimi wa ushairi wa Kiswahili
              ulipata mashiko katika karne ya kumi na nane (1700-1800). Katika kipindi hicho,
              kulikuwa na tungo kama vile Utenzi wa Hamziyya (bin Uthman, 1690), Utenzi
              wa Tambuka (Bwana Mwengo, 1728), Utenzi wa Al-Inkishafi (bin Nasir, 1800)
              na Utenzi wa Mwanakupona (Mwanakupona bint Mshamu, 1858). Tungo hizi
              zilitanguliwa  na tungo zilizohusu  simulizi  za Fumo Liyongo na zikafuatiwa
              na tungo za Muyaka bin Haji. Baada ya hapo, ulifuatia ukame wa tungo kwa
              kipindi cha takribani miongo mitano (1885 - 1945). Kulikuwa na tungo chache;
              ndiyo maana muhula wa pili unaitwa muhula wa utasa. Sababu za ukame huu ni
              pamoja na matukio ya vita yaliyotokea ulimwenguni. Baada ya hapo, ukafuatia
              muhula wa urasimi mpya ambapo kulikuwa na watunzi kama vile Shaaban
              Robert, Kaluta Amri Abedi na Mathias Mnyampala. Huu ni muhula ulioshuhudia
              kuimarishwa kwa kanuni za utungaji wa ushairi wa Kiswahili kama vile Sheria
              za Kutunga Mashairi na Diwani ya Amri (Abedi, 1954). Kisha, ulifuatia muhula
              wa sasa. Muhula huu ulianza wakati mataifa ya Afrika Mashariki yalipopata
              uhuru kutoka kwa wakoloni. Hiki ni kipindi kilichokuwa na wasomi wengi wa
              ngazi ya chuo kikuu waliojihusisha na utungaji, uhakiki na utafiti kuhusu masuala
              ya fasihi, ukiwamo ushairi. Hali hii mpya ilisababisha kuwapo kwa fikra mpya
              katika ushairi wa Kiswahili; ndipo ulipoibuka mjadala kuhusu ushairi usiofuata
              urari wa vina na mizani. Mjadala huo hujulikana kama Mgogoro wa Ushairi
              ambao umeelezwa kwa urefu katika kitabu cha Mulokozi na Kahigi (1982).



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            29
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   29                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   29
   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45