Page 44 - Fasihi_Kisw_F5
P. 44

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                               3.   Bado ungali kijana,
                                    Na dunia ngumu sana,

                                    Kukufunza kukuona,
          FOR ONLINE READING ONLY
                                    Ni jambo welekea.



                            Maisha Yangu na Baada ya miaka Hamsini (Robert, 1966: 6)
              Beti za hapo juu zinaonekana wazi kuwa zimeundwa na mishororo minne. Kina
              cha mshororo wa mwisho “a” ni tofauti na vina vya mishororo mingine mitatu
              katika beti zote.

              Ushairi wa maigizo
              Huu ni utanzu mmojawapo  wa ushairi wa Kiswahili. Utanzu huu tunaweza
              kuuweka katika michepuo miwili ambayo ni ngonjera na ushairi wa kidrama.

              (i)  Ngonjera
              Ngonjera ni aina ya ushairi andishi ambao huhusisha mabishano ya pande mbili.
              Upande unaojua  na ule  usiojua  jambo  fulani.  Kwa hiyo ushairi  wa ngonjera
              huandikwa kidayalojia ukihusisha pande mbili. Lengo kuu ni kuonesha udhaifu
              wa hoja kinzani kwa kuzikosoa hoja hizo ili, hatimaye,  hoja zilizolengwa
              zionekane kuwa na ushawishi mkubwa. Tazama mfano ufuatao wa ushairi wa
              beti chache za ngonjera:


                               Ngonjera ni kitu gani?

                               MDADISI
                               Ngonjera ni kitu gani, nasikia kila mara,

                               Yatamkwa midomoni, tena mbele ya hadhara,

                               Je, maana yake nini, nami nipate busara,
                               Maana yake ngonjera, nambie nami nijue.

                               JAWABU
                               Ngonjera zina kiini, cha mafunzo ya busara,

                               Mafunzo yenye kipini, cha kuamsha fikira,
                               Za mawazo akilini, na kugeuza majira,

                               Maana yake ngonjera, ni mafunzo kwa shairi.



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            33
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   33                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   33
   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49