Page 43 - Fasihi_Kisw_F5
P. 43

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Ukichunguza  beti  hizi  mbili,  utaona  kwamba hakuna  mizani  linganifu  wala
              urari wa vina. Kilichozingatiwa ni uteuzi wa maneno wenye kujenga picha na
              kumvutia msomaji au msikilizaji.


              Wanausasa  wanasisitiza  mshairi  awe na uhuru katika  kutunga  mashairi,  na
          FOR ONLINE READING ONLY
              kueleza mawazo yake bila kubanwa na kanuni za wanamapokeo. Kitu cha msingi
              katika shairi ni mpangilio wa maneno, lugha ya picha au taswira, tamathali za
              semi, hisia za kishairi na ujumbe.


              (b)  Tenzi
              Dhana ya tenzi imekwishaelezwa katika kipengele cha fasihi simulizi. Mambo
              machache ya kuyaongezea katika kipengele hiki ni kwamba, mara nyingi, tenzi
              huanza na dua, ambapo mwandishi humwomba Mungu amwongoze katika
              uandishi wake. Kwa kawaida, tenzi huwa na beti nyingi kuliko shairi la kawaida,
              lakini tenzi nyingi ni fupi kuliko tendi.

              Beti  za  utenzi  zinatakiwa  ziwe  hamsini  na kuendelea.  Hata  hivyo, urefu wa
              utenzi hutegemea uzito wa maudhui na ujuzi wa mwandishi. Aghalabu, mstari
              wa utenzi huwa nusu ya mshororo wa shairi la kimapokeo. Hivyo, utenzi huwa
              na mizani minane. Vilevile, vina katika mishororo mitatu ya kwanza, hufanana
              lakini mshororo wa mwisho huwa na kina tofauti. Kina hiki ambacho huitwa
              bahari hakibadiliki katika utenzi mzima. Tazama mfano katika baadhi ya beti za
              utenzi ufuatao:


                               Utenzi wa hati
                               1.   Leo nataka binti,

                                    Ukae juu ya kiti,

                                    Ili uandike hati,

                                    Ndogo ya wasia.




                               2.   Mimi kwako ni baba,
                                    Hati hii ya huba,

                                    Andika iwe akiba,

                                    Asaa itakufaa.




                32                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   32
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   32                    23/06/2024   17:54
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48