Page 47 - Fasihi_Kisw_F5
P. 47

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                         Yameshindwa chini kuzama, kwenye kina cha urazini,

                         Nao wahenga vibandani, nje tena hawatoki,


                         Hakuna tena ngoma, ya kugeana kani,
          FOR ONLINE READING ONLY
                         Na ushairi umehama, umerudi upeponi,

                         Lakini majani makavu, sasa hayatingishiki,

                         Nayo madirisha ya nyumba, imara yamefungwa,

                                 Waliomo ndani wahofu, hasira ya mizimu.

                                       Kichomi (Kezilahabi, 1988)

                         (i)  Toa maoni yako kuhusu hoja ya kuwa ili utungo uitwe shairi,
                              sharti ukidhi vigezo vya kauli 1(a)

                         (ii)  Tathmini  ukweli wa kinachosemwa  katika  kauli (b)
                              ukihusianisha na hali halisi ya sasa ya ushairi wa Kiswahili.


                 2.   Soma shairi la kisasa, kisha bainisha vipengele mbalimbali vya ushairi.

                 3.   Soma beti ishirini (20) za utenzi uupendao kisha chambua vipengele vya
                     fani na maudhui.

                 4.   Soma shairi lifuatalo, kisha jibu maswali yanayofuata.


                            Amina
                  1.  Amina umejitenga, kufa umetangulia,

                     Kama ua umefunga, baada ya kuchanua,

                     Nakuombea mwanga, peponi kukubaliwa,

                     Mapenzi tuliyofunga, hapana wa kufungua.

                  2.  Nilitaka unyanyuke, kwa kukuombea dua,

                     Sikupenda ushindike, maradhi kukuchukua,

                     Ila kwa rehema yake, Mungu amekuchagua,
                     Mapenzi tuliyofunga, hapana wa kufungua.




                36                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   36
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   36                    23/06/2024   17:54
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52