Page 50 - Fasihi_Kisw_F5
P. 50

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Hadithi fupi za kisiasa ni zile zinazohusu masuala ya kisiasa. Mifano ya hadithi
              hizo  ni  “Wali  wa Ndevu”  (Ruhumbika,  1974),  “Cha  Mnyonge Utakitapika
              Hadharani”,  “Magwanda  Kubilya  na  Vyama  Vingi”  na “Mayai  Waziri  wa
              Maradhi” (Kezilahabi katika Msokile, 1992).
          FOR ONLINE READING ONLY
              Hadithi fupi za kiutamaduni zinahusu masuala ya mila na desturi. Mifano ya
              hadithi fupi za kundi hili ni Tamaa Mbele (Banzi, 1970) na “Siku ya Mganga”
              (Mpilipili, katika Wamitila, 2012).


              Hadithi fupi za kifalsafa  huzungumzia  tafakuri kuhusu masuala mazito
              yanayomzunguka  mwanadamu  na ulimwengu  wake. Mifano ya hadithi
              fupi za kifalsafa ni “Wasubiri  Kifo” (Kezilahabi,  katika  Msokile, 1992) na
              “Mchakamchaka wa Maisha” (katika Komba, 1978).


              Hadithi fupi pendwa ni zile ambazo huzungumzia masuala yanayosisimua kama
              vile mapenzi, matukio yenye uajabu ajabu, mauaji na upelelezi. Mifano ya hadithi
              hizi ni “Sadiki Ukipenda” (Mohamed, 2002)


              Pamoja  na  uainishaji  wa hadithi  fupi  uliofanywa  hapo  juu, ni  vigumu  kuwa
              na hadithi fupi yenye maudhui ya mwelekeo mmoja. Hivyo, hadithi fupi moja
              inaweza kubeba maudhui ya aina mbalimbali.


               Shughuli ya 2.11
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, soma hadithi fupi zisizopungua nne (4) kisha,
              bainisha aina zake na chambua maudhui ya hadithi hizo.

               Shughuli ya 2.12
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, fafanua dhana na historia ya tamthiliya.

              Tamthiliya
              Tamthiliya  ni mchezo ulioandikwa ili utendwe jukwaani au usomwe, kwa
              malengo mbalimbali. Tamthiliya hujengwa na wahusika na migogoro iliyomo
              katika mchezo. Migogoro ndiyo hukuza mwendo wa tamthiliya kwa kutumia
              visa ambavyo hutendwa na wahusika mbalimbali.  Wahusika huzungumza na
              kutenda matendo mbalimbali kisanii.

              Historia ya tamthiliya
              Tamthiliya haikuwapo nchini Tanzania kabla ya ujio wa Waingereza. Ujio wao
              ulileta drama ambayo ndiyo chanzo cha tamthiliya. Drama iliingizwa shuleni na
              Waingereza kwa lengo la kuwaburudisha na kuwakumbusha utamaduni wao, hasa




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            39
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   39                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   39
   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54   55