Page 51 - Fasihi_Kisw_F5
P. 51

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              baada ya saa za kazi ambapo wengi wa walimu walikuwa Waingereza. Ilikuwa
              rahisi kuanzisha vikundi vya drama shuleni kwa sababu shule nyingi zilikuwa za
              bweni; na hivyo, wanafunzi walipatikana muda wote. Vilevile, wanafunzi hao
              walifahamu vizuri lugha ya Kiingereza. Tamthiliya nyingi zilizoigizwa ni zile
          FOR ONLINE READING ONLY
              zilizoandikwa na Waingereza. Miongoni mwa tamthiliya hizo ni The Merchant
              of Venice (Shakespeare, 1596) na Julius Caesar (Shakespeare, 1599). (Kwa kuwa
              tamthiliya hizi hazikuwa na uhusiano na mazingira ya Kitanzania, Watanzania
              walioziigiza waliona ni kiburudisho tu yaani tamthiliya hizo hazikuwa na maana
              kubwa kwao. Kadiri muda ulivyopita, baadhi ya Watanzania walivutika na sanaa
              ya tamthiliya. Hata hivyo, hawakuwa na ujuzi wa kuandika tamthiliya kama zile
              za  Waingereza. Miaka ya mwanzo baada  ya uhuru, maudhui  hayakubadilika
              mpaka lilipotangazwa Azimio la Arusha mwaka 1967. Maudhui ya tamthiliya
              ya baada ya Azimio la Arusha yalichukua sura mpya kwa kutangaza siasa ya
              Ujamaa na Kujitegemea kwa kuunga mkono au kukosoa.

              Tamthiliya  za mwanzo ziliathiriwa  sana na vichekesho. Pia, ziliathiriwa  na
              tamthiliya za Kiingereza. Watunzi walitunga tamthiliya zilizofanana kimaudhui
              na  zile  za  akina  Shakespeare.  Kwa mujibu  wa  Mazrui  (2007)  na  Mulokozi
              (2017), tamthiliya za mwanzo za Kiswahili zilitungwa nchini Kenya. Mifano ya
              tamthiliya hizo ni Mgeni Karibu (Hyslop, 1957), Nakupenda Lakini (Kuria, 1957)
              na Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi (Ngugi, 1961). Kwa upande wa Tanzania, miaka
              ya 1960, tamthiliya za Kiingereza zilitafsiriwa. Miongoni mwa tamthiliya hizo
              ni zile za Shakespeare za Juliasi Kaisari (Nyerere, 1964), Mabepari wa Venisi
              (Nyerere, 1969),  Tufani  (Mushi, 1969) na tamthiliya  ya Kiyunani  ya  Mfalme
              Edipode (Mushi, 1969). Tamthiliya nyingine ni zile zilizoandikwa na Waafrika.
              Zilizotafsiriwa ni Mtawa Mweusi (wa Thiong’o, 1970), Masaibu ya Ndugu Jero
              (Yahaya, 1974) na Nitaolewa Nikipenda (wa Thiong’o na wa Mirii, 1982).

              Kuanzia miaka ya 1960, watunzi wa Kitanzania  walianza  kutunga tamthiliya
              za Kiswahili kwa ajili ya Watanzania. Miongoni mwa watunzi waliojitokeza ni
              Ebrahim Husein ambaye tamthiliya yake ya kwanza ni, Wakati Ukuta (1967),
              ilishinda  na  kupata  tuzo  katika  mashindano.  Tamthiliya  nyingi  zilizotungwa
              miaka ya 1960 ziliigizwa  tu shuleni na katika kumbi za maonesho lakini
              hazikuchapishwa.

              Tamthiliya nyingi za Kiswahili zilichapishwa kama matokeo ya kuhitimu kwa watu
              wengi katika fani ya sanaa za maonesho katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
              Pia, yalikuwa ni matokeo ya kuanzishwa kwa mashindano ya uigizaji  miaka
              ya 1970 - 1990. Baadhi ya tamthiliya zilizochapishwa ni Kinjekitile (Hussein,



                40                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   40                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   40
   46   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56