Page 56 - Fasihi_Kisw_F5
P. 56

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Historia ya riwaya
              Riwaya ni utanzu wa hivi karibuni zaidi ukilinganishwa na ushairi na tamthiliya.
              Inadaiwa kwamba riwaya ilipata  umbo ililonalo  hivi sasa katika  karne ya 18
              huko Ulaya. Riwaya ilizuka kutokana na maendeleo na mageuzi ya kiutamaduni
          FOR ONLINE READING ONLY
              na viwanda. Ukoloni na “uvumbuzi”  viliumba  hali zilizohitaji  kuelezwa
              kwa mawanda mapana  kuliko  ilivyowezekana  katika ngano na hadithi  fupi.
              Uchangamani wa maisha katika nyanja mbalimbali kama vile siasa, utamaduni
              na uchumi ulihitaji kuwa na utanzu wa fasihi ulio na uchangamani kifani na
              kimaudhui pia. Kupanuka kwa usomaji, hasa wakati wa mapinduzi ya viwanda
              huko Uingereza, kuliwafanya waandishi waandike kazi ndefu kwa sababu
              walikuwapo wasomaji, hasa wanawake, waliokuwa wakibaki majumbani wakati
              waume zao wakiwa viwandani (Senkoro, 1984; Njogu na Chimerah, 1999;
              Madumulla, 2009).

              Afrika ni miongoni mwa mabara yenye historia fupi zaidi ya riwaya, ambapo
              maandiko ya riwaya yalianza kujitokeza mwishoni mwa karne ya 19. Katika eneo
              la Afrika ya Mashariki, kazi za kinathari za kwanza hazikukidhi ubora wa usanii
              na ubunifu. Baadhi ya maandiko ya awali ni Habari za Wakilindi (el Ajjemi, 1885,
              1907, 1962), Tulivyoona na Tulivyofanya Uingereza (Kayamba, 1933), Mwaka
              katika Minyororo (Sehoza, 1921) na Uhuru wa Watumwa (Mbotela, 1934). Vyote
              hivi vinaangukia katika kundi linaloendana na tawasifu au masimulizi ya wasafiri.
              Kwa hakika, kiwango cha usanifu wa vitabu hivi ni cha chini.

              Nchini Tanzania, kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazoendelea, nathari andishi
              ya kibunifu ni fani ambayo ilichelewa kuja. Nathari bunifu simulizi, kama vile
              hadithi, hekaya na ngano zilizosimuliwa kwa mdomo ndizo ambazo zilizotawala
              ndani ya jamii.


              Kwa upande wa fasihi andishi, kwa kipindi kirefu, maandiko ya fani ya ushairi,
              hususani tenzi za Kiswahili katika hati ya Kiarabu, ndiyo yaliyotamba katika eneo
              la Pwani ya Afrika ya Mashariki. Maandiko ya kinathari yalianza baada ya ujio
              wa wamisionari. Nathari simulizi inayojulikana kuandikwa na wenyeji ni Habari
              za Muma (bin Hemed, 1880), nayo ilichapishwa mwaka 1935 katika Mambo
              Leo, gazeti la Kiswahili lililovuma wakati wa ukoloni wa Waingereza. Nathari
              nyingine ni ile ya Habari za Wakilindi iliyoandikwa na Abdallah bin Hemed bin
              Ali el Ajjemy mzaliwa wa Zanzibar kwa baba wa Kiarabu na mama wa Kihehe,
              na ambayo juzuu ya kwanza ilichapishwa mwaka 1894, ya pili mwaka 1904 na ya
              tatu mwaka 1907. Kitabu hiki kilihusu masimulizi ya Wasambaa. Kumbukumbu
              nyingine  ni  zile  zilizohusu  Lamu  na  ambazo  zinasadikiwa  kuwa ziliandikwa



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            45
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   45                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   45
   51   52   53   54   55   56   57   58   59   60   61