Page 57 - Fasihi_Kisw_F5
P. 57

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              na Shaibu Faraji, na kuchapishwa na William Hichens (1928). Maandiko haya
              yalitokea wakati wa kipindi cha Wajerumani (Njogu na Chimerah, 1999).

              Baada tu ya Vita vya Kwanza vya Dunia, Waingereza walijishughulisha zaidi na
              kuandika na kufasiri vitabu vya shule vya kiada na ziada. Baadhi ya vitabu hivyo
          FOR ONLINE READING ONLY
              ni:  Hadithi ya  Allan Quartermain  (Haggard [mf.] Frederick Johnson,  1934),
              Safari za Gulliver (Swift, [mf.] Frederick Johnson, 1932), Mashimo ya Mfalme
              Sulemani (Haggard, [mf.] Edwin Brenn, 1929), Alfu Lela Ulela ([Waf.] Frederick
              Johnson na Edwin Brenn, 1929), na Kisiwa Chenye Hazina (Stevenson [mf.]
              Frederick Johnson, 1929). Maandiko haya yalikuwa maarufu hadi kufikia mwaka
              wa 1950 ambapo waandishi wazawa walianza kujitokeza kuandika nathari za
              kibunifu (bunilizi) kwa mfuatano wa kimikondo (Madumulla, 2009).

              Riwaya ya Kiswahili iliendelea  kukua na kubadilika  sambamba  na vipindi
              mbalimbali vya kihistoria nchini Tanzania. Katika kipindi cha miaka 1940 mpaka
              1970, riwaya za aina mbalimbali ziliandikwa, zikiwamo za kitawasifu, kimaadili,
              kiutamaduni, na za kihalifu au kikachero. Kwa mfano riwaya za kimaadili, zina
              sifa za kifasihi simulizi ambazo ni matumizi ya dialojia, kutofungwa na wakati
              pamoja  na matumizi  ya balagha  (chuku), ambayo  hukipatia  kitu sura, uwezo
              na nguvu isiyokuwa ya kawaida. Mifano ya riwaya hizi ni Kusadikika (Robert,
              1991), Kufikirika (Robert, 1968) na Adili na Nduguze (Robert, 1952).


              Riwaya za kiutamaduni  zilisheheni  maudhui yaliyosawiri tamaduni  za jamii
              mbalimbali.  Mfano mmojawapo ni riwaya ya  Kurwa na Doto (Farsy, 1960)
              inayosawiri maisha ya watu wa visiwa vya Unguja na Pemba. Halikadhalika,
              kuna riwaya ya Mzishi wa Baba ana Radhi (Nkwera, 1967), inayoelezea maisha
              ya Wapangwa wa mkoa wa Njombe, wilayani Lubewa. Vilevile, kuna riwaya
              ya Bwana Myombekere na Bibi Bugonoka, Ntulanalwo na Bulihwali (Kitereza,
              1980) ambayo inasawiri mila na desturi za jamii ya Wakerewe kabla ya kuja kwa
              wakoloni.

              Riwaya za kihalifu au kikachero zilibeba  maudhui ya uhalifu na upelelezi.
              Mifano mizuri ni riwaya za Muhammed Said Abdulla ambazo ni Mzimu wa Watu
              wa Kale (1957), Kisima cha Giningi (1968), Duniani kuna Watu (1973), Siri ya
              Sifuri (1974) na Mwana wa Yungi Hulewa (1976).

              Baada ya uhuru, na hatimaye Azimio la Arusha kutangazwa, ziliibuka riwaya
              zenye maudhui yanayohusu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Katika kipindi hiki,
              makundi mawili ya waandishi yalijitokeza kuandika riwaya kuelezea Azimio la
              Arusha. Kundi la kwanza liliuona ujamaa kwa jicho la ujadi. Kundi hili liliandika


                46                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   46                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   46
   52   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62