Page 61 - Fasihi_Kisw_F5
P. 61

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (f)  Riwaya za istiara
              Hizi ni riwaya za mafumbo ambazo umbo lake la nje ni ishara au kiwakilishi
              tu cha jambo jingine. Mifano mizuri ni riwaya za Kusadikika (Robert, 1991) na
              Kufikirika (Robert, 1968) ambazo huenda ni istiara kuhusu utawala wa mabavu
          FOR ONLINE READING ONLY
              wa kikoloni.

              (g)  Riwaya za kingano
              Hizi ni riwaya zenye umbo na mtindo wa ngano. Mathalani, huweza kuwa na
              wahusika wanyama, visa vya ajabuajabu, mandhari ya kubuni na visa vyenye
              kutendeka nje ya wakati wa kihistoria. Mfano wa riwaya za kingano ni Adili na
              Nduguze (Robert, 1952) na Lila na Fila (Kiimbila, 1966).

              (h)  Riwaya teti
              Hizi ni riwaya zinazosimulia  vituko na masaibu ya maayari  (watu wapuuzi,
              laghai, wajanja, na kadhalika) kwa njia inayosisimua na kuchekesha. Aghalabu
              maayari  hao huwa watu  wanaovutia  (si wahusika  wawi/waovu), wanatokea
              tabaka la chini, na bapa. Matukio ya riwaya hii hayana msuko ulioshikamana
              vizuri.

              (i)  Riwaya barua
              Hizi ni riwaya ambazo  sehemu yake kubwa husimuliwa  kwa njia  ya barua
              wanazoandikiana baadhi ya wahusika. Mfano ni riwaya ya Barua Ndefu kama
              Hii (Mariama Bâ, 2009).

              (j)  Riwaya za kihistoria
              Riwaya hizi huchanganya historia halisi na ubunifu ili kutoa maudhui fulani.
              Mara nyingi, riwaya hizi zinajikita  kwenye matukio makuu ya kihistoria
              yaliyoathiri mwenendo na mwelekeo wa jamii au taifa linalohusika. Riwaya ya
              kihistoria huchanganya wahusika wa historia na wa kubuni, matukio ya kweli
              na ya kubuni. Hata hivyo, riwaya hizo huzingatia zaidi namna matukio makuu
              ya kihistoria yalivyomwathiri mtu binafsi aliyeyashiriki. Riwaya ya kihistoria
              ina  dhamira  zinazogusa  watu  wengi,  ni  muhimu  kwa sababu  masimulizi
              yake yanahusu mambo yaliyotokea, na inawezekana  yaliwahi kuwapata hata
              wasomaji.  Ni kumbukumbu nzuri  ya  kipindi  kilichopita.  Baadhi  ya  riwaya
              mashuhuri za kihistoria ni Uhuru wa Watumwa (Mbotela, 1934), Kuli (Shafi,
              1979), Zawadi ya Ushindi (Mtobwa, 1987), Kwa Heri Iselamagazi (Mapalala,
              1992) na Pambazuko Gizani (Mboneko, 2004). Pia, kuna riwaya za Mulokozi za
              Ngome ya Mianzi (1990), Ngoma ya Mianzi (1991) na Moto wa Mianzi (1996).
              Nyingine ni Miradi Bubu ya Wazalendo (Ruhumbika, 1992) na Wachamungu wa
              Bibi Kilihona (Ruhumbika, 2014).


                50                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   50                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   50
   56   57   58   59   60   61   62   63   64   65   66