Page 59 - Fasihi_Kisw_F5
P. 59

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              ni Nyota ya Huzuni (Liwenga, 1978), Njozi Iliyopotea (Mung’ong’o, 1979), Sudi
              ya Yohana (Chachage, 1981), Kivuli (Chachage, 1981), Harusi (Safari, 1984) na
              Miradi Bubu ya Wazalendo (Ruhumbika, 1992).


              Riwaya hizo za kihakiki zimeendelea kuandikwa mpaka miaka ya 2000. Riwaya
          FOR ONLINE READING ONLY
              hizi zimejadili upokezi na athari za soko huria lililotokana na sera za ubinafsishaji.
              Katika  mfumo huu, njia kuu za uchumi  zinamilikiwa na watu binafsi, wengi
              wao  wakiwa  si  wazawa.  Kwa hiyo,  wazawa  wameendelea  kuishi  maisha
              magumu  kinyume  na matarajio  waliyokuwa  nayo, baada  ya uhuru, hususani
              baada ya kutangazwa kwa Azimio la Arusha. Mifano ya riwaya zenye maudhui
              yanayohusiana na ubinafsishaji na soko huria ni Almasi za Bandia (Chachage,
              1991) na Makuadi wa Soko Huria (Chachage, 2002).

              Ikumbukwe kwamba hakuna mpaka bayana katika vipindi vilivyotajwa hapo juu.
              Kuna kazi za fasihi andishi zenye maudhui yanayohusu vipindi tofauti katika
              kipindi kimoja. Hivyo, si ajabu kukuta riwaya za kiuhakiki katika kipindi cha
              Azimio la Arusha; vivyo hivyo, riwaya pendwa zinajitokeza katika vipindi vyote.
              Pia, hali hii inaweza ikatokana na mhamo wa kutoka kipindi kimoja kwenda kipindi
              kingine. Katika kipindi cha mpito, kunakuwa na kazi za fasihi zinazozungumzia
              kipindi ambacho kinaelekea kufikia mwisho na nyingine zinakuwa na maudhui
              ya kipindi kilichopo au hata kijacho.


              Aina za riwaya
              Riwaya hugawanywa kwa kuzingatia vigezo mbalimbali. Vigezo vilivyo maarufu
              ni vya kutazama fani na maudhui. Kifani, riwaya huainishwa kwa kuzingatia
              jinsi vipengele vya fani vinavyojitokeza.  Kadhalika, kimaudhui, mgawanyo
              hutazama mambo yanayoongelewa katika riwaya inayohusika. Kigezo hiki cha
              maudhui ndicho kinachotumika katika kitabu hiki. Kwa kutumia kigezo hiki,
              kuna makundi makubwa mawili ya riwaya: riwaya dhati na riwaya pendwa.

              1.  Riwaya dhati

              Riwaya dhati ni zile  zinazochambua  matatizo  au masuala mazito  ya kijamii,
              kutafuta sababu zake, athari zake na ikiwezekana ufumbuzi wake. Riwaya hizi
              hukusudiwa kumfikirisha msomaji kuhusu masuala mazito na si kumstarehesha
              tu. Riwaya dhati zimegawanyika katika aina mbalimbali. Aina hizo ni: riwaya
              za kijamii, kisaikolojia, sira, kiistiara, kingano, teti, chuku, kihistoria, kimaadili,
              kimapinduzi na kifalsafa. Pia, kuna riwaya za barua, vitisho na za watoto na
              vijalunga.





                48                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   48                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   48
   54   55   56   57   58   59   60   61   62   63   64