Page 55 - Fasihi_Kisw_F5
P. 55

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Sifa za riwaya
              Kuna sifa mbalimbali za riwaya. Kwa kawaida riwaya huwa:
              (a)  ndefu ikilinganishwa  na tanzu  nyingine.  Urefu wa riwaya  ya  Mungu

                   Hakopeshwi (Baharoon, 2021) kwa mfano, ni tofauti na ule wa hadithi fupi
          FOR ONLINE READING ONLY
                   ya Uwike Usiwike Kutakucha (Ruhumbika, 1978);

              (b)  na visa changamani, yaani huwa na visa zaidi ya kimoja, ambapo kisa kikuu
                   hujengwa na visa vidogo;

              (c)  na wahusika wengi na waliokuzwa. Kutokana na riwaya kuwa na visa vingi,
                   basi huwa na wahusika wengi ambao humwezesha mwandishi kukidhi haja

                   hii;

              (d)  na  mandhari pana  na huendelezwa  kikamilifu.  Kwa kuwa riwaya
                   hushughulikia  mawazo  mengi,  hujishughulisha  na vipengele  vingi  vya
                   maisha ambavyo hupatikana  katika nyakati na mahali tofauti kama vile
                   shuleni, mijini, vijijini, nyumbani na barabarani. Ili kushughulikia mazingira

                   mapana, simulizi hutumia kipindi kirefu cha wakati ikilinganishwa  na
                   kazi kama vile za hadithi fupi ambazo huweza kuchukua kipindi kifupi tu
                   kukamilika;

              (e)  na migogoro iliyokuzwa zaidi kwa sababu mwandishi ana uhuru mkubwa
                   wa kuiibua na kuieleza kwa kina;

              (f)  Hutumia lugha ya kisanii ya kinathari / lugha ya mjazo; na

              (g)  Kwa sababu ya urefu na upana wake, riwaya huwa na uwezo wa kubeba au
                   kutomelea tanzu nyingine (kama vile barua, insha, shairi, wimbo au igizo)

                   bila  matatizo. Mathalani, katika  riwaya  ya  Kiu ya Haki  (Mwanga,1983)
                   mwandishi ametumia hadithi ndani ya hadithi. Hadithi mojawapo ni ile ya
                   Mzee Fundisha anayesimulia yaliyompata alipovamiwa na polisi nyumbani

                   kwake na kulazimishwa  kutoa rushwa ya Sh. 2,000 ingawa hakuwa na
                   hatia. Vilevile, kuna hadithi ya Sikujua, anayesimulia yaliyompata miaka
                   kumi iliyopita wakati yeye na Pondamali wakifanya biashara ya kubadilisha
                   fedha.






                44                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   44                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   44
   50   51   52   53   54   55   56   57   58   59   60