Page 46 - Fasihi_Kisw_F5
P. 46

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                      Mfalme: Mwenzako lakini kakukosa nini?

                               Mwenzako kakufanya nini?
                               Mimi bado sijaamini
          FOR ONLINE READING ONLY
                               Kwa kweli baya mimi sijalibaini
                               Basi jambo hilo lanikata maini

                               Na kunivunjia matumaini

                               Mbona unaivunja ihsani

                               Yake sisi tul’omwamini


                            0Posa za Bikisiwa (Mohamed, 2013)

              Kwa jumla, kuna sifa mbalimbali za kisanaa zinazoutofautisha ushairi na tanzu
              nyingine za riwaya pamoja na tamthiliya.




                                Zoezi la 2.2


                 1.   Soma kauli hizi mbili kisha jibu maswali (a) na (b) yanayofuata:
                     (a)  “Katika kitabu hiki, tungo za Euphrase Kezilahabi,  Kulikoyela
                          Kahigi, Mulokozi na wengineo watungao tungo tutumbi zisizokuwa

                          na sanaa yoyote nimezitupa pembeni … Muundo wa mashairi yote
                          yaliyomo kitabuni humu ni ya asili ya Kibantu. Kila utungo wa
                          shairi umefungika upande wa mistari; umefungika upande wa vina;

                          ni lazima mistari iwe na vina; umefungika upande wa mizani; ni
                          lazima  kila  mstari  uwe na  idadi  sawa ya  mizani.  Mashairi  yote
                          yaimbwe; yaweza pia kusomwa au kusemwa tu. Tungo zisizotimiza
                          yote hayo si mashairi.”

                                 Mgogoro wa Ushairi na Diwani ya Mayoka (Mayoka, 1986)
                     (b)  Washairi wa mapokeo, sasa wacheza lala salama,

                          Katika mionzi hafifu, ya jua machweoni,

                          Na mahadhi yagaagaa, juu ya bahari ya utenzi,



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            35
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   35                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   35
   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51