Page 49 - Fasihi_Kisw_F5
P. 49

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Swahili Tales as Told by the Natives of Zanzibar (1870), Hekaya za Abunuwasi
              (1928) na Alfu Lela Ulela (1928). Hadithi hizi zilikuwa za kimapokeo na zenye
              kuingiliana na fasihi simulizi. Visa halisi vya kwanza katika hadithi za lugha
              ya Kiswahili vilianza miaka ya 1950 katika magazeti ya Mamboleo, Mwafrika,
          FOR ONLINE READING ONLY
              Baraza,  Nyota Afrika  na  Kiongozi. Katika miaka ya 1960, visa hivi vilianza
              kuchapishwa kwenye vitabu. Baadhi ya watunzi mashuhuri wa hadithi fupi za
              Kiswahili ni Gabriel Ruhumbika, Alex Banzi, Joseph Kiimbila, Kyallo Wamitila
              na Owen Onyango. Baadhi ya mikusanyiko ya hadithi fupi iliyochapishwa ni
              Misingi ya Hadithi Fupi (Msokile, 1992), Mwendawazimu na Hadithi Nyingine
              (Mbatiah,  2000),  Mimba Ingali  Mimba na Hadithi Nyingine,  (MacOnyango,
              2006),  Mizungu ya Manabii na Hadithi nyingine  (Habwe, 2010),  Shingo ya
              Mbunge na Hadithi Nyingine (Wamitila, 2010)


              Sifa za hadithi fupi
              Hadithi fupi huwa na sifa au kaida zinazoitofautisha na riwaya. Nazo ni kuwa na:


              (i)  urefu wa kusomeka kwa mkao mmoja. Kwa kawaida hadithi fupi haizidi
                   maneno 10,000;

              (ii)  muundo sahili;
              (iii)  wahusika wachache ambapo, aghalabu, mhusika mkuu huwa mmoja
                   au wawili.  Wahusika hawa hawakui kitabia  wala hawakui kulingana na
                   maendeleo ya kisa;

              (iv)  dhamira chache ikilinganishwa na riwaya. Mara nyingi, huwa na dhamira
                   kuu moja katika kisa kikuu kimoja; na

              (v)  mawanda finyu ya kiwakati na kijiografia.
              Aina za hadithi fupi
              Hadithi fupi huainishwa katika makundi mawili: hadithi fupi dhati na hadithi
              fupi pendwa. Hadithi fupi dhati huwekwa katika makundi yafuatayo: hadithi fupi
              za kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kifalsafa.

              Hadithi fupi za kijamii huzungumzia masuala mbalimbali ya kijamii kama vile
              ndoa, jinsia, mapenzi na malezi. Mifano ya hadithi fupi za kijamii ni: “Uwike
              Usiwike Kutakucha” (Ruhumbika), na “Siri ya Bwanyenye” (Mulokozi) zote
              hizi zimo katika Msokile (1992). Nyingine ni “Damu Nyeusi” (Walibora, 2007)
              na “Kijana Yule” (Mohamed, 2010).






                38                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   38                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   38
   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54