Page 39 - Fasihi_Kisw_F5
P. 39

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 2.8
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani eleza sifa za fasihi andishi na
              tanzu zake.

          FOR ONLINE READING ONLY
              Tanzu na vipera vya fasihi andishi
              Kama ilivyo kwa fasihi simulizi, fasihi andishi pia ina tanzu zake. Kwa mujibu
              wa wataalamu mbalimbali kama vile Wamitila (2002) na Mulokozi (2017) kuna
              tanzu nne za fasihi andishi ambazo ni ushairi, hadithi fupi, tamthiliya na riwaya.
              Kadhalika, tanzu hizo zimegawanyika katika vipera. Tazama Kielelezo namba
              2.2.

                                                  Fasihi Andishi





                      Ushairi              Hadithi fupi       Tamthiliya         Riwaya




                     Mashairi                Dhati              Tanzia             Dhati
                      Tenzi                 Pendwa              Ramsa             Pendwa
                Ushairi wa maigizo                            Melodrama
                    (ushairi wa
                ngonjera na ushairi                          Tanzia-ramsa
                   wa kidrama)


                                  Kielelezo namba 2.2: Tanzu za fasihi andishi


               Shughuli ya 2.9
              Kwa kutumia vyanzo vya maktabani au vinginevyo, jadili dhana na chimbuko la
              ushairi wa Kiswahili.

              Ushairi
              Mulokozi (2017) anaueleza ushairi kuwa ni “sanaa ya lugha ya mkato yenye
              ubunaji inayosawiri au kueleza jambo, hisi, hali au maono kwa namna yenye
              kuvutia hisia na katika mpangilio wa maneno wenye urari na wizani.” Inamaanisha
              kuwa ushairi husawiri mawazo, hisi au tukio kwa muhtasari katika mpangilio
              maalumu wa lugha teule ya kitamathali. Kwa hiyo, ushairi hutofautiana na tanzu
              nyingine za fasihi andishi katika umbo na matumizi ya lugha. Tanzu nyingine
              hutumia lugha ya mjazo ya kinathari lakini ushairi hutumia lugha ya mkato, yenye



                28                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   28
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   28                    23/06/2024   17:54
   34   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44