Page 36 - Fasihi_Kisw_F5
P. 36

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              maingiliano ya muda mrefu. Makabila yote ya Mkoa wa Mara, kwa mfano, ni
              watani wa Wanyaturu na Wanyiramba (Singida) na Wahaya (Kagera).


              Utani  hujenga uhusiano na  ushirikiano  mzuri  baina  ya wanajamii.  Vilevile,
              utani hutunza historia ya jamii zinazotaniana. Aidha, utani huwafunza watoto
          FOR ONLINE READING ONLY
              upendo na majukumu, mathalani, utani wa mjukuu wa kike na babu anapomwita
              mke wake na kuomba amfanyie jukumu fulani, mtoto huyo hujifunza jukumu
              lake  atakalolitekeleza  akiwa  mkubwa.  Vilevile,  utani  hukumbusha  wanajamii
              majukumu  yao. Mathalani, katika  misiba,  watani  hutumia  tukio  kukumbusha
              watu kujuliana hali wanapokuwa wazima na kusaidia kazi zihusuzo msiba. Kama
              zilivyo dhima nyingine za fasihi, utani huburudisha kwenye matukio ya furaha
              na  huzuni.  Ikumbukwe  kwamba,  utani  unaweza  kusababisha  ugomvi  endapo
              mhusika hajui kuwa anayemfanyia mzaha ni mtani wake.

              (f)  Maigizo
              Maigizo ni sanaa inayotumia watendaji kuiga tabia na matendo ya watu au viumbe
              wengine  ili  kuburudisha au kutoa  ujumbe  fulani.  Maigizo  haya  yanapoletwa
              jukwaani na kuoneshwa kwa hadhira huitwa drama. Mara nyingi, maigizo ya
              Kiafrika huambatana na utambaji wa hadithi, vichekesho, nyimbo, matendo ya
              kijadi kama vile harusi, jando na unyago. Wahusika hutakiwa kutumia lugha ya
              kifasihi inayoendana na hadhira. Zipo aina mbalimbali za maigizo, zikiwamo
              maigizo ya misibani na mivigani, maigizo ya watoto na ya burudani.

              (g)  Michezo ya watoto
              Watoto hucheza michezo mingi yenye kuambatana  na usanii. Michezo hiyo
              hutofautiana majina kulingana na mahali. Katika michezo hiyo, kuna kuimba,
              kucheza, kurukaruka, kukimbia, kughani, kujigamba na kuigiza. Baadhi ya
              michezo hiyo ni: kiota, ukuti, pembea (bembea), kitikiti, kibuzi na kombolela.
              Aghalabu, michezo hiyo huambatana na nyimbo, majibizano, vitendo na maigizo.
              Kwa mfano,  katika  mchezo  wa  kiota,  watoto  hunyanyuka  pale  walipoketi  na
              kuanza kutangatanga huku na huku ilihali wakiimba mpaka kila mmoja anapopata
              mahali pake na kukaa. Watoto huimba hivi:

              Kiota
              Sisi ndege twaruka

              Twatafuta kiota
              Kiota

              Kiota
              Kiota



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            25
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   25                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   25
   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41