Page 33 - Fasihi_Kisw_F5
P. 33

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Wakati  wa ukoloni, sanaa za  jadi,  hasa zile  zilizohusiana  na imani  za dini,
              zilipigwa vita. Hali hii ilisababisha sanaa kama vile matambiko kupotea katika
              baadhi  ya jamii.  Sanaa nyingine  zimedumu  mpaka  leo kutokana  na wito wa
              kitaifa wa kudumisha utamaduni wa Kitanzania na uimara wa jamii wa kutunza
          FOR ONLINE READING ONLY
              utamaduni wao.

              Sanaa za maonesho mamboleo ni zile zilizotokana na athari za ujio wa wageni.
              Sanaa za namna hii ni vichekesho na maigizo.


              Majigambo
              Majigambo ni masimulizi ya kujisifia au kujikweza kwa mtu kuhusu mambo
              aliyowahi kufanya. Mambo hayo huwa ni ya kishujaa kama vile kupigana vita,
              kuua wanyama wakali au kufanya jambo lolote kubwa la kishujaa. Kwa kawaida,
              majigambo husimuliwa katika lugha ya kishairi na yanaweza kujitokeza katika
              fasihi andishi na fasihi simulizi, zikiwamo bongo fleva na taarabu. Mjigambi
              hufanya matendo mbalimbali.  Aghalabu, mjigambi  hubeba silaha kama vile
              mkuki na ngao au upinde na mishale. Kama mjigambi ametoka kuua simba, kwa
              mfano, ataonesha matendo ya jinsi alivyopambana na simba hadi kumshinda.

              Makabila yenye sanaa za majigambo ni yale ya Ukanda wa Ziwa (kama vile
              Wakurya, Wasukuma na Wahaya), yale ya Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania,
              hususani Wahehe, na ya Kaskazini mwa Tanzania, hasa Wamasai. Majigambo
              hufanyika wakati wa sherehe za harusi na za kuwapokea au kuwapongeza
              mashujaa. Pia, hufanyika kwenye mikutano inayoitishwa na watawala. Majigambo
              huambatana na ngoma na nyimbo za kusifu. Mjigambi hutokea katika kikundi
              kinachocheza na kujigamba. Baada ya kumaliza, mjigambi mwingine hufuata.
              Mara nyingi, mjigambi  wa mwisho huwa yule aliyetenda jambo la kishujaa
              kuliko wote au yule anayeijua vizuri sanaa ya majigambo.

              Lengo kuu la majigambo ni kujenga ari ya ushujaa, ukakamavu na ujasiri. Mtu
              anayefanya kitendo cha kishujaa, hushangiliwa na kupewa heshima kubwa katika
              jamii yake. Kwa msingi huu, vijana huhamasika kuwa wajasiri na wakakamavu
              ili kulinda hadhi na heshima ya jamii zao. Ijapokuwa, wajigambi wengi kwa
              kawaida, huonekana kuwa wanaume hasa katika ngoma za kujigamba na kwenye
              vikao vya pombe hata wanawake hujigamba katika miktadha tofauti ikiwamo ile
              ambayo inawahusisha wanawake peke yao. Mfano mzuri ni katika taarabu, hasa
              zile za mipasho. Kwa ujumla, majigambo hulenga kudumisha utu na heshima ya
              mtu katika jamii.






                22                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   22                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   22
   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37   38