Page 30 - Fasihi_Kisw_F5
P. 30

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                               Shida yako ni rupia, takujalia fulusi
                               Hebu njoo Jumamosi, bado nashauri moyo

                               Mkopaji
          FOR ONLINE READING ONLY
                               Hodi Bwana nawasili, kwa ile yetu miadi
                               Unihesabie mali, arubani nakidi
                               Muaminishe Jalali, nifanyie itikadi
                               Tafadhali nikopeshe, haondoe shida yangu

                               Mkopwaji
                               Moyo wangu siamini, kukuhesabia mali
                               Shuruti lete dhamini, ambaye msema kweli

                               Shilingi arubaini, kulipa huna dalili
                               Hebu njoo Jumapili, bado nashauri moyo



                              Ngonjera za Ukuta: Kitabu cha kwanza (Mnyampala, 1967:22)

              (c)  Tenzi
              Tenzi ni tungo ndefu zinazoeleza tukio fulani linalotokea au lililowahi kutokea
              katika jamii; au zinazofafanua jambo au fikra fulani. Tenzi huwa na kisa kimoja
              kinachoelezwa  kwa kina. Kisa hicho kinaweza kuwa maelezo  kuhusu wasifu
              wa mtu fulani, jambo fulani la kihistoria au jambo lolote. Sifa ya kusimulia au
              kuelezea jambo kwa urefu ndio husababisha tenzi kuwa na beti nyingi kuliko
              mashairi au aina nyingine za ushairi.

              Utendi  ni utungo wenye masimulizi  marefu kuhusu matendo ama matukio
              ya kishujaa na wasifu wa mashujaa. Utenzi na tendi huwa na muundo wenye
              kufungamana na mahadhi ya ala ya muziki inayotumika au melodia ya uimbaji.
              Kwa kawaida, hazina urari wa vina na mizani. Tenzi zenye urari wa vina na mizani
              ni zile zenye kufuata kanuni za ushairi andishi wa Kiswahili japo chimbuko au
              utungaji wake ni wa kisimulizi. Mifano ya tenzi hizo ni Utenzi wa Nyakiiru Kibi
              (Mulokozi, 1997) na Utenzi wa Mwanakupona. Mfano wa tendi ni Utendi wa
              Fumo Liyongo (Kijumwa, 1913) katika Tenzi Tatu za Kale (Mh. Mulokozi, 1999).
              Katika tenzi hizo, mishororo haikugawanywa katika vipande viwili. Kila ubeti
              huwa una mistari minne; mistari mitatu ya kwanza ikiwa na vina vyenye urari na
              ule wa mwisho ukiwa na kina tofauti. Pamoja na vina hivyo kuwa na urari sawa,
              hubadilika toka ubeti mmoja hadi ubeti mwingine. Kina kinachorudiwa katika




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            19
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   19                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   19
   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35