Page 28 - Fasihi_Kisw_F5
P. 28

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Ushairi simulizi hujipambanua na tanzu nyingine za fasihi simulizi kutokana na
              matumizi ya mizani, lugha ya mkato, lugha ya mafumbo na uimbaji au ughani.
              Mbali na kuzingatia mambo hayo yanayohusu ushairi kwa jumla, ushairi simulizi
              una sifa ya kutungwa papo kwa papo na kufungamana na muktadha au tukio
          FOR ONLINE READING ONLY
              mahususi. Vipera vya ushairi simulizi ni nyimbo, mashairi, ngonjera, maghani
              na tenzi. Wakati mwingine, mashairi huambatana na ala za muziki za jadi ama
              za kisasa.

              (a)  Nyimbo
              Nyimbo ni tungo za kishairi zinazowasilishwa kimuziki kwa kutumia sauti iliyo
              katika mpangilio fulani wa mahadhi na melodia, na inayozingatia mapigo ya
              kiurari. Mahadhi au tuni ni sauti mahususi ya uimbaji wa wimbo fulani, na melodia
              ni mpangilio na mwendo wa uimbaji wenye kuzingatia urari wa mapigo au ridhimu
              aghalabu hutofautiana kati ya jamii moja na nyingine. Nyimbo huweza kuimbwa
              na kuchezwa pamoja na ala za muziki. Nyimbo huimbwa na mtu mmoja au kundi
              la watu. Wakati mwingine, kikundi cha waimbaji huwa na kiongozi na wafuasi
              wake. Kiongozi huanzisha wimbo, halafu wafuasi huitikia mkarara. Kiongozi
              wa nyimbo huitwa manju. Nyimbo zinaainishwa kwa kuzingatia dhima, hadhira
              inayoimbiwa  na  muktadha unaofungamana  nazo.  Kutokana  na  vigezo  hivyo,
              tunapata baadhi ya aina kama ifuatavyo: tumbuizo, bembezi, kongozi, nyimbo za
              dini na wawe. Yafuatayo ni maelezo mafupi kuhusu aina hizi:

                   (i)  Tumbuizo ni nyimbo za furaha ziimbwazo katika matukio mbalimbali
                        kama vile harusini na ngomani.

                   (ii)  Bembezi/chombezi ni nyimbo za kubembelezea watoto.

                   (iii)  Kongozi ni nyimbo za kuaga na kukaribisha mwaka.
                   (iv)   Nyimbo za dini ni nyimbo zinazoimbwa kwa lengo la kumsifu Mungu
                        au miungu.

                   (v)  Wawe  ni nyimbo  za  kilimo  zinazopatikana  karibu  katika  makabila
                        yote ya Tanzania.

                   (vi)  Mbolezi ni nyimbo zinazoimbwa kufuatia matukio ya huzuni, hasa ya
                        vifo.

                   (vii) Nyimbo za watoto ni nyimbo zenye maudhui mahususi kwa ajili ya
                        watoto.






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            17
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   17                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   17
   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33