Page 24 - Fasihi_Kisw_F5
P. 24

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Kwa mfano, kigano kinaweza kueleza kuhusu mzazi aliyempenda mno mtoto
              wake wa pekee kiasi cha kutothubutu kumkemea au kumrudi. Hatimaye, mtoto
              alijenga  tabia  mbaya. Basi, msimulizi  husema kwa methali:  Mchelea  mwana
              kulia hulia mwenyewe.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Aghalabu, vigano hutokea katika mazungumzo na, wakati mwingine, hutungwa
              papo hapo. Kwa  mantiki  hiyo, vigano vingi huwa havienei kwa sababu
              hufungamanishwa na muktadha wa maongezi na hutungwa kwa ajili ya mada
              husika tu. Kwa hiyo, hupotea baada ya mada kuwasilishwa.

              (e)  Soga
              Soga ni hadithi fupifupi za utani na ucheshi. Hadithi hizi husimuliwa kwa
              mfuatano wa matukio yanayochekesha. Soga hujengwa juu ya tukio moja tu.
              Tukio hilo, aghalabu, hulenga kuchekesha kwa kubeza na kukejeli. Pia, hueleza
              mambo ya ukweli unaoumiza kwa njia ya ucheshi ili kupunguza ukali wa ukweli
              huo. Soga hupatikana au hufanywa na watu wa jamii zenye historia ya kufanyiana
              utani kama vile jamii za Wanyaturu na Wakurya, Wahaya na Waha, Wachaga na
              Wapare. Kwa ujumla, soga hujikita katika kuburudisha na, wakati mwingine,
              kuelimisha jamii. Tazama mfano wa soga inayowahusu Wamakonde hapa chini:

              Kisa cha Mmakonde na Ngedere
               Mmakonde mmoja  alikwenda shambani  kwake, akamkuta  ngedere  akila
               mahindi shambani mwake. Ngedere alipomwona Mmakonde akakimbilia juu
               ya mti. Mmakonde akamwona kule alikojificha, akamwambia: “Wee ngedere
               nimechakuona;  uchijifanye  n’janja,  telenka  hapa chini  nikupige  nchale  ili
               upate adhabu moja tu. Vinginevyo, n’kupige nchale ukiwa hukohuko juu ya
               nti, upate adhabu mbili: Adhabu ya kupigwa nchale, na adhabu ya kuanguka
               kutoka juu ya  nti  baada ya kupigwa  nchale. Je, wewe ungekuwa ngedere
               ungefanyaje?


               Shughuli ya 2.3
              Tumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, kufafanua semi na vipera vyake kwa
              kuzingatia maana na sifa.


              Semi
              Semi ni tungo fupifupi za fasihi simulizi, na aghalabu, hutumia picha, tamathali
              na ishara. Semi hutumika  kutoa mafunzo, nazo zimegawanyika  katika  vipera
              mbalimbali kama vile methali, misemo, mizungu, mafumbo, na vitendawili.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            13
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   13                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   13
   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29