Page 19 - Fasihi_Kisw_F5
P. 19

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (a)  Ngano
              Ngano ni hadithi  za kimapokeo  zitumiazo  wahusika kama wanyama, miti  na
              watu. Ni kipera cha mwanzo kabisa katika utanzu wa hadithi. Kwa kawaida,
              mtunzi wa ngano hajulikani. Ngano hupokezanwa na kuendelezwa kutoka kizazi
          FOR ONLINE READING ONLY
              hadi kizazi. Maudhui yake hujikita katika maadili, uhusiano na mwenendo mzuri
              katika jamii. Aghalabu, ngano ni hadithi za burudani ambazo husimuliwa katika
              mazingira ya starehe na mapumziko. Ngano ina vipera vidogo kadha. Baadhi ya
              vipera hivyo ni kisasuli, hurafa, hekaya na istiara.

              Kisasuli
              Kisasuli ni hadithi ya kisanaa yenye kueleza usuli na sababu za jambo, tukio
              au hali. Mathalani, zipo hadithi zinazoeleza kwa nini mnyama fulani anapenda
              kushirikiana na wanadamu au ameumbika kwa namna fulani. Tazama mfano wa
              kisasuli cha hadithi ya “Kwa nini nyoka hana miguu?”


                Kwa nini nyoka hana miguu?
               Siku moja Nyoka pamoja na wanyama wengine walialikwa kwenye sherehe
               nyumbani  kwa mfalme.  Kule walikula  na kunywa! Baadaye  mfalme
               aliwaita ili wapewe zawadi. Kwa sababu ya uroho wake, Nyoka hakusikia
               wito. Alipozinduka, alikuta miguu yote, hata ile hafifu ya Tandu na Buibui,
               imeshatolewa; akabakia anajiburuza kwa tumbo lake. Mpaka leo hii nyoka
               hana miguu (Balisidya, 1987).


              Hurafa ni ngano zenye wahusika wanyama tu. Wanyama hao huwakilisha tabia
              na matendo ya binadamu kwa kurejelea masuala yanayopatikana katika jamii.
              Maudhui katika hurafa hueleza kuhusu tabia nzuri au mbaya za binadamu, kama
              vile woga, ulafi na tamaa. Katika hurafa, wanyama wanaotumiwa ni kama vile
              sungura, fisi na kobe. Sungura huwakilisha ujanja, kutokata tamaa na kutochoka.
              Fisi  huwakilisha  tamaa,  ulafi,  woga,  uzembe  na  ujinga.  Kobe  huwakilisha
              ukimya, busara na utulivu. Aidha, ni mhusika ambaye hufanya vitu kimyakimya
              lakini huibuka mshindi. Ufuatao ni mfano wa hurafa:

              Sungura na Fisi
               Siku moja Sungura alipokuwa matembezini alikutana na Fisi. Fisi alimwangalia
               Sungura na kumuuliza, “Wewe unayekodoa macho hivi unaenda wapi, au kuila
               nyama yako?” Sungura akamwangalia Fisi na kumwambia, “Nimeambiwa na
               Simba nimsubiri hapa ndipo tuandamane hadi kwake nikamtayarishie ini la
               Fisi analolitamani sana.” Fisi akamwangalia Sungura na kumwuliza, “Huyo
               Simba yuko wapi?” Sungura akaita kwa sauti ya juu, “Simbaaaaaa!”



                 8                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   8
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   8                     23/06/2024   17:54
   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24