Page 15 - Fasihi_Kisw_F5
P. 15

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Wachambuzi wengine wenye mtazamo wa kidhanifu ni Felician Nkwera na John
              Ramadhan. Katika insha yake kuhusu fasihi, Nkwera (1976) anasema “Fasihi ni
              sanaa ambayo huanzia kwa Muumba, humfikia mtu katika vipengele mbalimbali...
              (ni) hekima  ambayo mtu ameshirikishwa  apate  kumtambua  Muumba wake”.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Akiunga mkono mtazamo huo, Ramadhan (1975) anasema kwamba, ingawa fasihi
              ni hisi, kitendo cha mtu kuibuni kazi ya sanaa ni uigaji wa Mungu ambaye ndiye
              mfalme wa sanaa zote. Mawazo ya wafuasi wa nadharia hii hayana uthibitisho
              wowote zaidi ya kumtenga msanii na jamii yake kwa kumkweza na kuonekana
              yuko karibu na Mungu kuliko wanajamii wengine. Aidha, wafuasi wa nadharia
              hii wanaamini kuwa mwanafasihi hawezi kubuni kitu chochote zaidi ya kuiga
              sanaa ambayo tayari Mungu ameitengeneza.

              Nadharia ya kiyakinifu
              Kwa mujibu wa Senkoro (1987), chimbuko la sanaa na fasihi ni mazingira
              halisi ya jamii, hususani sanaa ya mwanzo iliyofungamana na kazi za uzalishaji
              mali. Hii inamaanisha kwamba chanzo cha fasihi na sanaa ni binadamu (jamii)
              na mazingira  yake. Katika  harakati  za kukabili  mazingira  yake, ilimlazimu
              binadamu kufanya kazi. Binadamu wa mwanzo aliishi katika mazingira yasiyo
              rafiki. Hivyo, ilimlazimu kutumia silaha ili apambane na mazingira hayo. Huo
              ndio ulikuwa mwanzo wa kutafuta njia za kurekebisha silaha zake (mawebutu)
              kwa kuyachonga ili yawe na ncha kali. Uchongaji huo ndio ulikuwa sanaa
              yenyewe. Kwa hiyo, hisia za kisanaa zimefungamana  na maendeleo  ya mtu
              katika kupambana na mazingira yake na katika kufanya kazi. Nadharia hii ina
              mwelekeo wa kukubalika zaidi, kwani inakubaliana na fikra kuwa wanadamu
              walianza mawasiliano kupitia kazi zao. Kwa mantiki hiyo, chimbuko la sanaa ni
              kazi.

              Kadiri binadamu  alivyozidi kuendelea,  alikuwa na mahitaji mengine  zaidi  ya
              mahitaji  ya  msingi.  Mahitaji  hayo  yaliamsha  hisia  za  kuchora  vielelezo  vya
              shughuli zake za kujikimu. Michoro ya mapangoni iliyopo Kondoa (Tanzania) ni
              mifano mizuri ya vielelezo hivyo. Kuzuka kwa lugha kuliongeza aina nyingine
              ya sanaa ambayo ni fasihi.

              Fasihi, kama zilivyo  sanaa nyingine, ilitokana  na kazi alizofanya  binadamu
              katika kupambana na mazingira yake. Fasihi ilianzia katika wimbo wa kazi.
              Baadaye, tanzu nyingine za fasihi zilitungwa na kusimuliwa kwa madhumuni
              ya kufunza, kukosoa, kuadibu, kuchokoza fikra na kuliwaza jamii baada ya kazi.
              Kadiri maendeleo ya uzalishaji mali yalivyoongezeka, binadamu akapata muda
              wa kupumzika na kustarehe kwa njia ya sanaa. Fasihi ilianza kutengana na kazi



                 4                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   4                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   4
   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20