Page 12 - Fasihi_Kisw_F5
P. 12

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari







                    Sura
                      ya              Dhana na chimbuko la fasihi
                            Maisha bila FasihiREADING ONLY
                  Kwanza






                          Utangulizi

               Fasihi  inatuwezesha  kufikiri  kwa  kina  na  kufahamu  tamaduni  na  masuala
               mbalimbali ya kijamii pamoja na kuwasiliana kwa ufasaha. Katika sura hii,

               utajifunza juu ya dhana ya fasihi, mitazamo mbalimbali ya dhana hiyo ya
               fasihi, na chimbuko la fasihi. Umahiri utakaojenga katika sura hii utakusaidia
               kukuza uelewa na kutathmini maarifa hayo.




          FOR ONLINE





               Shughuli ya 1.1
              Kwa kutumia vyanzo vya maktabani, mtandaoni, au vinginevyo, bainisha matini
              ambazo unadhani ni fasihi, na eleza kwa nini unadhani hivyo.


              Dhana ya fasihi
              Wataalamu mbalimbali wameielezea dhana ya fasihi kwa namna tofauti. Kwa
              ujumla wanakubaliana  kuwa fasihi ni sanaa bunifu ya lugha inayosawiri hali
              mbalimbali za maisha. Hali hizi ni pamoja na mahusiano, hisia za watu, mazingira,
              migogoro na mengineyo. Sanaa ya fasihi inajidhihirisha katika tanzu kama vile
              tamthiliya, riwaya, ushairi, semi na nyinginezo.
               Shughuli ya 1.2

              Kwa kutumia mifano ya fasihi unayoifahamu, toa maoni yako kuhusu dhana ya
              fasihi.

               Shughuli ya 1.3
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, fafanua mitazamo kuhusu dhana ya fasihi.


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            1
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   1                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   1
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17