Page 13 - Fasihi_Kisw_F5
P. 13

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mitazamo mbalimbali kuhusu dhana ya fasihi
              Kuna mitazamo mbalimbali inayojadili dhana ya fasihi. Mtazamo wa kwanza
              unajiegemeza  kwenye kisawe cha neno fasihi kwa kiingereza, yaani literature.
              Mtazamo huu unadai kuwa literature ni jumla ya maandishi yote yaani kila kitu
          FOR ONLINE READING ONLY
              kilichoandikwa ni fasihi. Mtazamo huu umeelezewa na Wellek na Warren (1986),
              Hata hivyo, dhana hii inapingwa na baadhi ya wanazuoni wa fasihi. Kwa mfano,
              Mulokozi (2017) anadai  kuwa dhana ya  literature inatofautiana  na dhana  ya
              fasihi. Katika lugha ya Kiingereza, maana moja wapo ya literature ni maandishi
              yoyote, ilhali katika Kiswahili, dhana ya “fasihi” inazingatia fasihi kama sanaa
              na aina zote za fasihi.

              Mtazamo wa pili unadai kuwa fasihi ni hisi ambazo zinajifafanua kwa njia ya
              lugha. Wafuasi wakuu wa mtazamo huu ni Sengo na Kiango (1975). Wataalamu
              hawa wanasema kuwa ili mwanafasihi aweze kuandika au kueleza jambo kifasihi
              lazima  aguswe na  hisia  fulani. Wataalamu  hao  wanasema  kuwa hisi  ni kama
              kusikia njaa, baridi, joto, uchovu au kuumwa. Mtazamo huu pia umekosolewa na
              baadhi ya wanazuoni. Kwa mfano, Mulokozi (2017) anaeleza kuwa mtazamo huu
              unachanganya mambo matatu ambayo ni fasihi yenyewe, mambo yaelezwayo
              na fasihi, na mtindo wa kifasihi. Kwa mujibu wa mtazamo huu, fasihi inaweza
              kuelezea hisi lakini fasihi yenyewe si hisi. Kwa mfano, fasihi huweza kuelezea
              hisi za mapenzi lakini fasihi yenyewe si mapenzi.

              Mtazamo wa tatu unaitazama fasihi kama sanaa ya lugha yenye ubunifu bila
              kujali kama imeandikwa au la. Mtazamo huu unaafikiwa na Kirumbi (1975),
              Mutembei  (2006) na Senkoro (2011). Kwa mujibu  wa  mtazamo  huu,  hata
              nyimbo na masimulizi ya kisanaa ni fasihi, ijapokuwa hayakuandikwa. Kirumbi
              anasema kuwa fasihi ni taaluma ya sanaa inayowasilishwa kwa njia ya lugha
              katika muundo wa maandishi au matamshi. Senkoro (2011) ana mtazamo sawa
              na wa Kirumbi anapoieleza fasihi kuwa ni “sanaa itoayo maudhui yake kwa
              kutumia lugha ya maneno ambayo hutamkwa ama huandikwa.”


              Mtazamo wa nne unadai kuwa fasihi ni maandiko bora ya kisanaa yenye manufaa
              ya kudumu. Akizungumzia mtazamo huu, Summers (1989) anasema kuwa fasihi
              ni sanaa inayojumuisha zaidi maneno yaliyoandikwa. Mtazamo huu unaupa uzito
              ufundi wa kubuni lakini unafinya mawanda ya fasihi kwa kuhusisha  mawazo
              yaliyo bora tu ambayo, hata hivyo, ni vigumu kuyaainisha.

              Mtazamo wa tano unaeleza kuwa fasihi ni matokeo ya matumizi ya lugha kwa
              njia isiyo ya kawaida ili kuleta athari maalumu. Miongoni mwa waasisi wa mtazamo
              huu  Roman  Jakobson. Mtazamo huu huona  kuwa  fasihi  hukiuka  taratibu  za


                 2                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   2                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   2
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18