Page 14 - Fasihi_Kisw_F5
P. 14

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kawaida  za  matumizi  ya  lugha  katika  sarufi,  maana  na  sauti  ili  kumvutia  na
              kumuathiri msikilizaji au msomaji. Mtazamo huu humfanya msomaji aitafakari
              lugha yenyewe badala  ya kuutafakari  ujumbe  unaowasilishwa na lugha hiyo.
              Vilevile, fasihi inaonekana kuelemea zaidi upande wa fani na kupuuza maudhui,
          FOR ONLINE READING ONLY
              maana na muktadha wa kazi za fasihi.

              Kutokana na mjadala huu, tunaweza kusema kuwa mitazamo hii yote inahusisha
              fasihi, maisha na jamii. Yaani, fasihi ni sanaa inayotumia lugha kuwasilishia hali
              mbalimbali  zinazomhusu mwanadamu na maisha  yake. Tunaposema  “lugha”
              hatuna maana ya usemaji wa kutumia sauti tu, bali hata mawasiliano ya kutumia
              ishara na vitendo.

               Shughuli ya 1.4
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, jadili ubora na upungufu wa kila mtazamo
              kuhusu dhana ya fasihi.


                                Zoezi la 1


                1.   Ni kwa vipi si kila andiko ni fasihi?

                2.   Eleza ni kwa namna gani fasihi ni sanaa.

                3.   Jadili umuhimu wa fasihi katika maisha ya mwanadamu.


              Nadharia za chimbuko la fasihi

               Shughuli ya 1.5
              Soma matini  mbalimbali  zinazopatikana  mkondoni  na maktabani  zinazohusu
              nadharia za chimbuko la fasihi, kisha zielezee kwa ufupi.

              Dhana ya nadharia
              Wataalamu wanaeleza kuwa nadharia ni maelezo au mwongozo uliopangwa ili
              kusaidia kueleza, kutatua au kutekeleza jambo fulani. Nadharia za chimbuko la
              fasihi ambazo Senkoro (1987) na Mulokozi (2017) wanazitaja ni nadharia za
              kidhanifu na kiyakinifu.


              Nadharia ya kidhanifu
              Msingi wa nadharia hii ni mawazo ya kudhani, yasiyotokana na uhalisi. Waasisi
              wa nadharia hii ni wanafalsafa wa Kiyunani, wakiwamo Plato na Sokrate. Wafuasi
              wa nadharia hii wanaamini kuwa fasihi na sanaa vimetoka kwa Mungu. Hivyo,
              mwanafasihi huipokea sanaa ikiwa tayari imeivishwa na Mungu.


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            3
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   3                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   3
   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19