Page 16 - Fasihi_Kisw_F5
P. 16

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              za uzalishaji na kuanza kuwa shughuli maalumu ya kijamii ambapo ilitendwa
              katika matukio mbalimbali, kama vile sherehe na ibada.


              Nadharia  nyingine  inayoelezwa  na  Mulokozi  (2017) ni  ya  mwigo  au  uigaji.
              Nadharia hii inazingatia  ubunifu wa mwanadamu katika kuiga maumbile  na
          FOR ONLINE READING ONLY
              mazingira yaliyomzunguka kwa kusawiri vitu vilivyomo katika hali mbalimbali.
              Akigusia dosari kuu ya nadharia hii, Mulokozi anasema kuwa katika kusisitiza
              mno uigaji, suala la ubunifu wa kisanaa na kifasihi linasahauliwa.

               Shughuli ya 1.6

              Jadili ubora na upungufu unaojitokeza katika nadharia za chimbuko la fasihi.

                Tamrini

                1.   Kwa kutumia mifano, fafanua maana ya dhana zifuatazo:
                     (a)  Fasihi


                     (b)  Mtazamo

                     (c)  Nadharia

                     (d)  Chimbuko


                2.   Dhana ya fasihi huelezwa kwa mitazamo mbalimbali. Jadili mitazamo
                     hiyo.

                3.   “Ujifunzaji wa fasihi hauna umuhimu wowote.” Jadili hoja hii.

                4.   Chunguza fasili za dhana ya fasihi zifuatazo kisha, eleza zinafanana na
                     kutofautiana katika vipengele vipi?

                     (a)  Fasihi inahusisha ufundi wa matumizi ya lugha katika kuwasilisha
                          dhana na matukio mbalimbali yanayomhusu binadamu na
                          mazingira yake (Ponera, 2014).

                     (b)  Fasihi ni sanaa ya lugha yenye ubunifu inayosawiri vipengele vya

                          maisha, mahusiano, mazingira na hisia za watu katika muktadha
                          fulani (Mulokozi, 2017).

                     (c)  Fasihi ni sanaa itumiayo lugha ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa
                          na unaoendana na jamii husika (Mlaga, 2017).



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            5
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   5                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   5
   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21