Page 20 - Fasihi_Kisw_F5
P. 20

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Baada ya kuita kwa sauti hiyo, Sungura alijigeuza kidogo, akapiga mluzi na
               kusema kwa sauti nzito, “Naja sasa hivi. Naandama nyayo za Fisi aliyepita
               hapa. Natamani kumkamata ili nipate ini lake nikuletee ukanitayarishie kama
               tulivyoagana.  Mara tu  Fisi alipoyasikia  hayo, aligeuka  na  kutimua  mbio
          FOR ONLINE READING ONLY
               kuelekea kichakani. Sungura alibaki alikokuwa na kuangua kicheko.

              Hekaya ni ngano zenye visa visivyo vya kawaida vinavyoambatana na masaibu
              na pengine hata ujanja wa mhusika mkuu ambaye huweza kuwa mtu au mnyama.
              Hekaya hujengwa na visa vingi vinavyotofautiana. Mhusika mkuu katika hekaya
              hupitia misukosuko mingi hadi kukaribia kushindwa. Hata hivyo, katika hatua za
              mwisho kabisa, mhusika huyu huweza kuibuka mshindi kwa namna isiyotarajiwa.

              Lengo la hekaya ni kumtia mtu moyo asikate tamaa anapopitia changamoto za
              aina mbalimbali. Kimsingi, kinachohimizwa ni kutumia akili kutatua matatizo ya
              maisha. Kwa kumtumia mhusika sungura, kwa mfano, tunahimizwa kuwa wajanja
              na kutokujidharau hata kama ni wadogo. Umbile dogo linaweza kuwakilisha pia
              uwezo wa kiuchumi kama vile kuwa na mtaji mdogo. Mtu anaweza kutumia
              mtaji mdogo kufanya biashara mpaka kufikia kiwango cha kuwa mfanyabiashara
              mkubwa. Ufuatao ni mfano wa hekaya:

                Mfanyabiashara na Wakeze

               Hapo zamani,  kulitokea  mfanyabiashara  mmoja  aliyekuwa  na  mali  nyingi
               sana. Basi alioa mke, baadaye akaongeza mke wa pili (Bi mdogo). Wakaishi
               hivyo. Alitokea  kumpenda  zaidi  Bi. Mdogo na kumnyanyasa  Bi. Mkubwa
               (mke wa kwanza).

               Siku moja, alikuwa na safari ya kwenda kununua bidhaa za duka lake. Basi
               akamwambia Bi. Mdogo ataje mahitaji yote ambayo angependa aletewe kama
               zawadi. Bi. Mdogo akataja vitu vingi. Naam, kwa kuwa mfanyabiashara yule
               alikuwa akimpenda sana, hakusita kumhakikishia kwamba angemletea. Kwa
               shingo upande, alimwendea vilevile Bi. Mkubwa na kumwambia ataje zawadi
               ya kumletea. Yule Bi. Mkubwa akamwambia mumewe asisumbuke ila amletee
               pete na kipande cha akili. Basi, kwa dharau yule bwana akakubali.

               Basi  tajiri  yule  akafunga  safari  akafika  huko,  akanunua  vifaa  vyake  vyote
               alivyovihitaji kwa ajili ya duka lake. Vilevile, akanunua vitu vyote kama vile
               nguo ambazo  Bi.  Mdogo alimtuma,  pamoja  na  pete  ya  Bi.  Mkubwa. Sasa
               akakwama wapi apate kipande cha akili. Akazunguka maduka yote, asipate.
               Mwishowe, akaona ni upuuzi kuendelea kutafuta kipande hicho.



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            9
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   9                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   9
   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25