Page 21 - Fasihi_Kisw_F5
P. 21

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari





               Basi, katika  ghadhabu yake, akawa akimtukana  huyo Bi. Mkubwa, jinsi
               alivyokuwa mpumbavu. Ikatokea  kwamba Bi. Kizee mmoja  akamsikia
               alivyolalamika  na kuapiza.  Yule Bi. Kizee  akamuuliza  kwa nini  alikuwa
               akilalamika.  Yule  bwana akamsimulia  kisa chote.  Bi. Kizee  akamwambia
          FOR ONLINE READING ONLY
               yule  bwana  kuwa asipate  taabu  kwani  kipande  hicho  anacho  nyumbani.
               Wakafuatana kuelekea nyumbani kwa huyo Bi. Kizee. Kufika karibu na kule
               nyumbani, Bi. Kizee akamweleza kwamba kipande hicho kiko nyumbani kwa
               yule bwana, ila tu akitaka kukipata sharti atakapokaribia nyumbani kwake
               ajipake kinyesi, halafu aone jinsi wake zake watakavyompokea.

               Basi  tajiri  akafanya  kama  alivyoagizwa.  Alipokaribia  nyumbani  kwake,
               akajipaka  kinyesi mwili mzima,  akawa hovyo kabisa kisha akabisha hodi
               kwanza nyumbani kwa Bi. Mdogo. Bi. Mdogo kufungua mlango  katika
               harakati za kumlaki, akaona mumewe kajaa kinyesi mwili wote. Bi. Mdogo
               akafoka sana na kumwambia asithubutu kuingia mle ndani hadi awe ameoga
               vizuri.


               Basi yule bwana katika hali hiyohiyo, akaenda kwa Bi. Mkubwa. Bi. Mkubwa
               akamwona mumewe katika hali ile, akasikitika sana. Akamvua nguo zenye
               kinyesi, akamwosha, na kumvika nguo nyingine.


               Ndipo yule bwana akamwambia mke wake, “Pete na kipande cha akili vyote
               nimepata.  Isipokuwa kipande cha akili  nimekipata  hapahapa.” Akachukua
               zawadi zote, hata zile za Bi. Mdogo, akampa yule Bi. Mkubwa, na kumfukuza
               Bi. Mdogo.

               Wakaishi raha mustarehe.


              Riwaya ya Kiswahili (Madumulla, 2009: 94 - 95)

              Istiara ni hadithi ambayo maana yake ya wazi inawakilisha maana iliyofichika.
              Kwa  hiyo,  maana  huwasilishwa  kwa  njia  ya  mafumbo.  Kwa mfano,  hadithi
              mashuhuri ya zimwi linalovamia kijiji na kuwameza wanakijiji wote isipokuwa
              mwanamke mmoja mjamzito ni istiara. Katika hadithi hiyo, mama huyo mjamzito
              baadaye  anajifungua  mtoto  na  kumlea  akiwa  mafichoni.  Mtoto  anapokua
              anamuuliza  mama  yake kwa nini wako peke yao kijijini,  wakazi  wengine
              walikwenda wapi. Mama yake anamweleza kuwa watu wote walimezwa na zimwi
              ambalo linaishi katika msitu ulio karibu na kijiji hicho. Mtoto anaamua kwenda
              kupambana na zimwi hilo hadi analiua. Baada ya kuliua analipasua tumbo na
              kuwatoa watu wote waliomezwa wakiwa bado hai. Watu wanafurahi na kumfanya


                10                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   10
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   10                    23/06/2024   17:54
   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26