Page 26 - Fasihi_Kisw_F5
P. 26

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (c)  Mizungu
              Mizungu  ni  kauli  zenye  mafumbo  zinazoonesha  ukinzani  wa  fikra  au  tukio.
              Mbali na vitendawili vya kawaida, kuna vitendawili vingine vijulikanavyo kama
              mizungu. Mizungu hii hutumia zaidi mafumbo. Kwa mfano, inaelezwa kwamba
          FOR ONLINE READING ONLY
              mtu hawezi kumwoa ndugu wa damu. Ukinzani huu umetumika kuonya ndugu
              wasiwe na uhusiano wa kimapenzi. Mizungu hutumia mafumbo ya hali ya juu,
              kwa hivyo hutumiwa na watu wazima katika miviga ili kueleza dhana na mawazo
              mbalimbali  kwa maongezi  au  nyimbo.  Mifano  mizuri  ya mizungu  inayohusu
              jambo hili ni:

              (i)  Ua zuri sana limeota kwenye miiba; hivyo, huwezi kulichuma.

              (ii)  Papai limeiva nyumbani, ila siwezi kulila.
              Mizungu  hutumia  lugha  ya  picha  inayoonesha  ukinzani  wa  fikra.  Ukinzani
              husaidia kumfikirisha msikilizaji na kumpa changamoto ya kutafuta jibu. Mifano
              mizuri ya mizungu ni:


              (i)  Adui rafiki (moto)
              (ii)  Nimezishika lakini siwezi kuzitumia (mhasibu na fedha)

              (d)  Mafumbo
              Mafumbo ni kauli au maelezo yanayoficha maana ambayo humtaka msikilizaji
              kuyafumbua. Kwa mfano, watu wanamteta mtu, ikitokea mtetwaji anakuja mahali
              hapo, mmoja wao anaweza kusema wifi kaja au shangazi kaja. Hii huwasaidia
              kubadilisha  maongezi  baada ya kufumbua  wifi  au  shangazi  kuwa ndiye mtu
              anayetetwa ingawa mtu huyo si wifi wala shangazi wa mtu yeyote katika kundi
              hilo.

              Aidha,  kwenye  mazingira ambapo  watu  wanaongea  lakini  hawataki  mmoja
              wao ajue maongezi yao, labda kwa sababu ni domokaya, mmoja wao anaweza
              kuwatahadharisha  wenziwe kwa kusema hivi,  Ooho! Mkorosho umeanguka!
              Inabidi  waelewe kwamba “mkorosho ulioanguka” ni mmoja  wao. Hivyo,
              wataongea kwa tahadhari kubwa. Aghalabu, mafumbo mengi huwa ni kejeli dhidi
              ya watu wenye tabia mbaya. Mafumbo yana malengo ya kuelimisha, kuwezesha
              mawasiliano, kuburudisha, kukosoa na kuonya kuhusu mambo yanayotendeka
              miongoni mwa wanajamii.


              (e)  Vitendawili
              Vitendawili ni semi fupifupi za mafumbo zenye kutumia lugha ya picha, tamathali
              na  ishara  kueleza  jambo  lililofichika.  Jambo  hilo  ndilo  jibu  la  fumbo.  Kwa


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            15
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   15                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   15
   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31