Page 25 - Fasihi_Kisw_F5
P. 25

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (a)  Methali
              Methali ni semi za kimapokeo zenye hekima na busara zinazoelezea falsafa na
              uzoefu  wa jamii  fulani  kwa muhtasari.  Semi  hizi  hubeba  maana  pana  kuliko
              maneno yenyewe yanayotumiwa. Methali hutumika kusisitiza, kuelimisha,
          FOR ONLINE READING ONLY
              kuonya au kupongeza  kwa njia  za busara. Aghalabu, methali  hujengwa  kwa
              sitiari. Sitiari hizo hujitokeza katika pande mbili za methali ambazo hubainishwa
              kwa mkato. Angalia mifano ifuatayo:

                   (i)  Mtaka yote kwa pupa / hukosa yote.

                   (ii)  Usipoziba ufa / utajenga ukuta.

                   (iii)  Aisifuye mvua / imemnyea.

                   (iv)  Chanda chema / huvikwa pete.
                   (v)  Mtaka cha uvunguni / sharti ainame.

              Mifano ya hapo juu inaonesha kuwa methali hubeba dhima mahususi. Kwa mfano,
              methali (i) inawaasa wanajamii kutofanya mambo mengi kwa wakati mmoja. Ni
              vyema kumakinikia jambo moja ili kulifanya kwa ufanisi, ndipo uanze jambo
              jingine. Katika mfano wa (ii), jamii inaaswa kurekebisha tatizo katika hatua za
              mwanzo, yaani kabla madhara makubwa hayajatokea.


              (b)  Misemo
              Misemo ni tungo zitumiazo picha, ishara na tamathali kueleza kitu au wazo kwa
              ufupi ili kuelimisha au kuadilisha. Misemo hufananisha maisha na matukio au
              vitu. Wakati mwingine, misemo hutumika kutambulisha mazingira maalumu au
              kuijulisha hadhira kuhusu hali fulani ya kijamii. Angalia mifano ifuatayo:

              (i)  Bendera hufuata upepo.
              (ii)  Elimu ni bahari.

              (iii)  Ukubwa jalala.

              Mfano wa (i) unaonesha hali ya maisha, kwani wapo watu ambao hufuata mkumbo
              bila kufikiria wala kuhoji kwa nini wanafanya jambo fulani na, hatimaye, kujikuta
              kwenye matatizo. Katika mfano wa (ii), elimu inafananishwa na bahari. Bahari
              ni kubwa, na haina mwisho, vivyo hivyo kwa elimu. Elimu hutupatia maarifa na
              ujuzi wa aina mbalimbali. Pia, elimu haina ukomo, kwani binadamu hujifunza
              kila siku. Mfano wa (iii) unalinganisha hali ya mtu kuwa mkubwa wa umri au
              cheo, na kutupiwa lawama hata kama hajatenda kosa, kama lilivyo jalala ambapo
              watu hutupa taka za aina mbalimbali.



                14                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   14
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   14                    23/06/2024   17:54
   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30