Page 29 - Fasihi_Kisw_F5
P. 29

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Mashairi
              Mashairi ni tungo zenye kuelezea au kuonesha kwa ufupi wazo au jambo au
              hisi fulani  kuhusu binadamu  na mazingira  yake. Mambo hayo huelezwa
              katika  mpangilio  maalumu wa maneno fasaha yenye muwala,  aghalabu  kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              lugha ya kitamathali yenye kugusa moyo. Tunaposema mpangilio wa maneno
              tunamaanisha kuwa mpangilio wa maneno katika shairi hufuata kanuni tofauti na
              ule wa nathari. Si lazima shairi kufuata kanuni za miundo ya sentensi inayotumika
              katika  lugha husika. Mathalani,  badala  ya kuandika  usikate tamaa maishani
              huweza kuandikwa  maishani usikate  tamaa - mpangilio  ambao  ni tofauti  na
              mpangilio wa kawaida. Baadhi ya tungo za taarabu ni ushairi simulizi.

              Ngonjera
              Ngonjera ni neno la Kigogo lenye maana ya “twende pamoja” au “tuambatane.”
              Kipera hiki kilikuwapo toka zamani ila kilihuishwa mwishoni mwa miaka ya
              1960 na Mathias Mnyampala katika harakati zake za kuelezea siasa ya Ujamaa
              na Kujitegemea.


              Ngonjera ni mazungumzo au majibizano ya kishairi kuhusu mada fulani. Kwa
              kawaida, ngonjera haziimbwi, hughaniwa. Aghalabu, majibizano hayo huwa na
              washiriki wa pande mbili, upande wa wanaopinga na upande wa wanaotetea hoja.
              Wahusika hawa hutumia lugha ya kiishara pamoja na miondoko ya mwili kama
              vile mikono, macho na midomo. Kutokana na wahusika kutumia miondoko,
              ngonjera  huitwa ushairi wa maigizo.  Katika  ngonjera, suluhisho hupatikana
              mwishoni mwa majibizano,  ambapo  pande mbili  zinazopingana  hukubaliana.
              Ingawa ngonjera za Mathias Mnyampala ni fasihi andishi, lakini zinaweza
              kutendwa jukwaani. Mfano mzuri ni ngonjera ya Mkopo wa Fedha ya Mathias
              Mnyampala inayopatikana katika kitabu cha Ngonjera za Ukuta. Ngonjera hiyo
              ni majibizano ya papo kwa papo.



                               Mkopaji
                               Hodi Bwana nimekuja, nina shida na tatizi
                               Nijile kutaka haja, arubani ghawazi
                               Tazileta kwa pamoja, siku mbili zizi hizi
                               Tafadhali nikopeshe, haondoe shida yangu

                               Mkopwaji

                               Nimekwisha kusikia, tuliza yako nafusi
                               Haja nitakukidhia, Inshallah kitu hukosi



                18                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   18
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   18                    23/06/2024   17:54
   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34