Page 32 - Fasihi_Kisw_F5
P. 32

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Beti hizi ni sehemu ya simulizi ya kiutendi inayomhusu Fumo Liyongo. Simulizi
              hii  inaakisi  maudhui  ya kipindi  cha  miaka  ya 900-1500 BK. Hivyo, lugha
              iliyotumika ni ile inayoakisi kipindi hicho. Pia, simulizi katika utendi huu inahusu
              masuala kama vile nguvu za kimwili, kiakili, kisihiri, kivita na kiume (urijali).
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 2.5
              (a)  Tunga kazi kwa kutumia kipera kimojawapo cha ushairi.

              (b)  Chagua suala mtambuka mojawapo katika jamii kisha andaa majigambo.

               Shughuli ya 2.6

              Jadili sanaa za maonesho kwa kuzingatia maana, aina na sifa zake.

              Sanaa za maonesho
              Balisidya  na  Muhando  (1976)  wanadai  kwamba  sanaa  za  maonesho  ni  sanaa
              ambazo huwasilisha wazo ana kwa ana kwa kutumia usanii wa utendaji. Utanzu
              huu hujumuisha kipera chochote chenye mambo yafuatayo:


              (i)  Dhana ya kutendeka (tendo);
              (ii)  Mtendaji (fanani);

              (iii)  Uwanja wa kutendea (jukwaa);

              (iv)  Watazamaji (hadhira); na
              (v)  Kusudio la kisanaa (maudhui).

              Sanaa za maonesho huwa kwenye umbo linalotendeka. Huweza kugawanyika
              katika makundi mawili ambayo ni sanaa za maonesho za jadi na sanaa za
              maonesho mamboleo. Sanaa za maonesho za jadi ni zile zilizochipuka katika
              jamii za Kiafrika. Sanaa hizi hujumuisha majigambo, miviga, vichekesho,
              ngomezi, tambiko, utani, maigizo na michezo ya watoto. Ingawa miviga kama
              vile ibada, sherehe, jando na unyago ni matukio ya kijamii  au kimila  yenye
              kuvuka mipaka ya kisanaa, lakini inajumuishwa hapa kwa kuwa sanaa hutawala
              utendaji na uwasilishaji wa maudhui yake. Wakati wa uwasilishaji wa shughuli
              hizi, watu hufanya vitendo vya kisanaa kama vile uigizaji wa visasili, uchezaji
              ngoma, uimbaji na utongoaji mashairi, vikiambatana na matendo ya mwili. Kwa
              njia hii, watu huweza kuwasiliana wao kwa wao au kuwasiliana na miungu.
              Ijapokuwa dhima ya sanaa hizi hufanana kwa namna ya jumla, huwa kuna tofauti
              mahususi katika vipengele vya utendaji kati ya jamii au kabila moja na jingine.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            21
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   21                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   21
   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37