Page 34 - Fasihi_Kisw_F5
P. 34
Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari
(a) Matambiko
Matambiko ni ibada zinazoambatana na utoaji wa sadaka kwa Mungu, miungu na
mizimu. Tangu zamani, jamii mbalimbali zilifanya matambiko ili kutoa shukrani,
kusifu, kuomba msamaha na kadhalika. Tambiko ni tukio halisi ambalo baadhi
ya matini zinazotumika huwa na maneno ya kisanaa. Licha ya matumizi ya
FOR ONLINE READING ONLY
lugha ya kisanaa kama vile tamathali za semi, taswira na lugha ya mafumbo
kwa ujumla, matini za ushairi wakati mwingine husheheni nduni za ushairi ndiyo
maana linaingizwa katika kundi la sanaa za maonesho. Kwa kawaida, matambiko
hufanywa na watu maalumu katika jamii. Matambiko hufanyika katika maeneo
maalumu. Kwa mfano, watambikaji katika baadhi ya jamii za Kanda ya Ziwa
huelekeza maombi yao kwa Namhanga (Mungu Mkuu), Mugasa (mungu wa
wavuvi) au Kalungu (mungu wa wawindaji). Utendaji wa tambiko hili huenda
sanjari na matumizi ya maleba, vyungu na pembe maalumu. Sadaka zitolewazo
na jamii ya Wakerewe hujumuisha kuku, mbuzi, kondoo, ng’ombe, vyakula vya
nafaka na pombe huitwa empahe.
(b) Miviga
Miviga ni sherehe au shughuli zinazofanywa na jamii katika kipindi maalumu
cha mwaka au katika muktadha maalumu. Sherehe hizo zinaweza kuwa za jando
na unyago, harusi, au kutawazwa kwa Mtemi. Miviga ni sherehe zihusuzo mtu
kutoka katika kundi au wadhifa fulani na kuingia katika wadhifa mwingine.
Mathalani, anaweza kutoka katika rika la utoto kwenda ujana (jando na unyago)
na ujana kwenda utu uzima (kuoa au kuolewa). Kadhalika, miviga ni matendo ya
kimila ambayo wakati mwingine huhusisha sehemu kubwa ya jamii.
Miviga huambatana na maigizo na nyimbo zinazoendana na tukio husika. Katika
harusi, nyimbo zinazoimbwa ni za ndoa; na katika mazishi nyimbo zinazoimbwa
ni za maombolezo. Katika miviga, ngoma mbalimbali huchezwa. Aghalabu,
wazee hutoa mafunzo na mawaidha, hususani kwa watoto na vijana.
(c) Vichekesho
Vichekesho ni aina ya sanaa ya fasihi simulizi. Katika sanaa hii, watu husimulia
visa na mikasa ambavyo huwafanya wasikilizaji na watazamaji wacheke.
Vichekesho vinahitaji ubunifu mkubwa ili kupata jambo litakaloibua hisia na
kuvunja mbavu. Lugha inayotumika katika vichekesho ni nyepesi na iliyojaa
picha ambazo watazamaji wana uwezo wa kuzitambua. Hii ni kwa sababu
hutumia mifano ya vitu vinavyojulikana wazi kwa hadhira au vinavyopatikana
katika mazingira yao. Aidha, vichekesho hutumia mbinu ya kejeli, dhihaka na
utani.
Kitabu cha Mwanafunzi 23
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 23 23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 23