Page 27 - Fasihi_Kisw_F5
P. 27

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kawaida, kitendawili hupewa jibu kwa neno moja au zaidi au maelezo. Kama
              ilivyo katika kazi nyingine za fasihi, vitendawili hutumika kuburudisha, kukuza
              uwezo wa kufikiri, kupamba lugha, kukosoa au hata kukejeli. Tazama mifano
              ifuatayo:
          FOR ONLINE READING ONLY
              (i)  Pango langu limejaa mawe - kinywa.
              (ii)  Nyumba yangu ina nguzo moja - uyoga/mwavuli.

              (iii)  Blanketi la babu lina chawa - mbingu na nyota.

              (iv)  Bibi amejitwisha machicha ya nazi - mvi.
              Uundaji  wa vitendawili  hutegemea  mazingira  ambako  kitendawili  hicho
              hutumika. Tazama mifano ifuatayo:


              (i)  Watoto wa sultani wamevaa kofia.
              (ii)  Nimenunua sungura nimemvika kofia.

              (iii)  Nikune kichwa nikupe moto.

              Jibu la vitendawili hivi vyote ni njiti ya kiberiti.

              Tofauti ya vitendawili vya (i), (ii) na (iii) inatokana na mazingira. Kitendawili cha
              (i) kimeundwa katika mazingira ambayo sultani aliwahi kuishi. Kitendawili cha
              (ii) kimeundwa katika sehemu yenye wafugaji au pori lenye sungura. Kitendawili
              cha (iii) kimeundwa katika mazingira yanayoakisi udugu, ambapo ni rahisi mtu
              kuomba kukunwa kichwa.

               Shughuli ya 2.4
              Tumia maktaba au maktaba mtandao na vyanzo vinginevyo kujadili maana, sifa
              na vipera vya ushairi simulizi.


              Ushairi simulizi
              Ushairi simulizi ni utanzu wa fasihi simulizi ambao huwasilishwa kwa hadhira
              kwa njia ya uimbaji au ughani badala ya usemaji wa kawaida. Ushairi simulizi
              ulianza  wakati binadamu  alipoanza  kufanya kazi.  Kupitia  lugha, binadamu
              alibuni nyimbo za kazi. Nyimbo hizo ndizo msingi wa fasihi simulizi. Nyimbo za
              kazi zilitungwa kwa kuzingatia mapigo ya zana za kazi ili ziweze kukumbukwa
              kwa urahisi.







                16                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   16                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   16
   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32