Page 22 - Fasihi_Kisw_F5
P. 22

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              mtoto huyo kuwa kiongozi wao. Kiistiara, hadithi hii huweza kuwakilisha ukoloni
              na mapambano ya kujikomboa. Zimwi linamwakilisha mkoloni, na mtoto ni
              mkombozi. Pia, hadithi hii inaweza kuwa ishara ya kupigania haki ya aina yoyote
              (Thomas, 2011)
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kwa kawaida, ngano huwa fupi kwa sababu ya muundo wake wa kuwa na kisa
              kimoja. Wahusika wa ngano ni bapa kwa maana kwamba mhusika akiwa mwema
              ni mwema mwanzo hadi mwisho wa hadithi, vivyo hivyo kwa mhusika mwovu.
              Lengo kuu la ngano, mbali na kuburudisha, ni kuadibu, kuadili na kuelimisha
              jamii. Hujaribu kujenga utu bora kwa kueleza wema na ubaya.


              (b)  Tarihi
              Tarihi ni hadithi zinazohusu matukio muhimu ya kihistoria. Msingi wa hadithi
              hizi ni matukio ya kihistoria. Matukio haya yanaweza kuwa ya kweli au ya
              kubuni au mchanganyiko wa ukweli na ubunifu. Aghalabu, wahusika wa hadithi
              hizi ni binadamu. Miongoni mwa mifano maarufu ya tarihi ni Tarihi ya Kilwa.
              Tazama mfano ufuatao:


              Mji wa Kilwa na Watawala Wake
               Hapo awali,  Mji  wa Kilwa  ulikuwa  ukitawaliwa  na  Waswahili  wenyewe.
               Kiongozi wa mwisho kabla ya ujio wa wageni alijulikana  kwa jina la
               Mndimbo. Alitawala mpaka karne ya saba. Watawala waliofuata walikuwa
               wenye asili ya Kiarabu. Sultani wa kwanza, Ali bin-Hasan, alianza kutawala
               mwaka 1200BK. Inasemekana alitengeneza sarafu ya kwanza. Utawala wake
               ulifuatiwa  na al-Hasan bin Daudi, ambaye  alikuwa mjukuu wa Ali, lakini
               wengine walipinga kwa kuwa alikuwa mpwa wake na utawala wake ulikoma
               miaka ya 1300BK. Utawala mwingine ulianza mwaka 1300 ambapo al-Hasan
               bin Talut alianza kutawala. Al-Hasan bin Talut alikuwa mtawala wa kwanza
               katika ukoo wa tawala za Abu’ l-Mawahibu. Alikuwa na sarafu chache sana
               zinazoashiria kipindi kifupi cha utawala wake. Mtoto wake aliyeanza kutawala
               alijulikana kwa jina la Sultani Sulaiman bin al-Hasan. Isivyo bahati, mtawala
               huyu haoneshwi katika orodha za Masultani katika fasili ya Kiarabu ingawa
               kuna sarafu nyingi ambazo zinasemekana zilikuwa zake. Alishika madaraka
               kwa miaka miwili tu. Mwaka 1320 al-Hasan bin Sulaiman alianza kutawala.
               Mtawala huyu alitembelewa na Ibn Batuta mnamo mwaka 1331. Inasemekana,
               huyu ndiye aliyejenga husuni kubwa na alikuwa na sarafu nyingi. Kuna habari
               kuwa Mafia ilichukuliwa na Kilwa katika utawala huu. Mtawala aliyefuata
               ni  Daudi  bin  Sulaiman;  huyu  alikuwa  ndugu  wa al-Hasan  bin  Sulaiman.
               Inasemekana alikuwa na sarafu chache sana na ndiye mtawala wa mwisho
               kutengeneza sarafu kabla ya ujio wa Wareno (Massamba, 2017).



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            11
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   11                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   11
   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27