Page 17 - Fasihi_Kisw_F5
P. 17

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari






                    Sura

                      ya                   Fasihi simulizi na fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
                     Pili                                andishi






                          Utangulizi

               Fasihi simulizi na fasihi andishi ni sanaa muhimu ambazo mtu huzitumia kwa
               malengo ya kujiburudisha, kuelimisha na hata kuhifadhi utamaduni wa jamii.
               Katika sura hii, utajifunza kuhusu tanzu na vipera vya fasihi simulizi na fasihi
               andishi na pia utajifunza uhusiano uliopo baina ya fasihi simulizi na fasihi
               andishi. Aidha, utajifunza kuhusu mchango wa fasihi simulizi katika maendeleo
               ya fasihi andishi na mchango wa fasihi kwa jumla katika maendeleo ya jamii.
               Umahiri utakaoujenga katika sura hii utakusaidia kuchambua na kutathmini
               vipengele mbalimbali katika maisha.





                            Nyenzo ya kuwasilisha mawazo katika miktadha mbalimbali




               Shughuli ya 2.1
              Kwa kutumia vyanzo vya mkondoni na maktabani, chunguza tanzu na vipera vya
              fasihi simulizi kisha jibu maswali yafuatayo:
              (i)  Nini tofauti ya utanzu na kipera?

              (ii)  Kuna tofauti gani kati ya utani na majigambo?

              (iii)  Kuna tofauti gani kati ya utanzu wa hadithi na semi?
              (iv)  Sanaa za maonesho zina sifa zipi?

              (v)  Nini tofauti ya misemo na misimu?

              Tanzu na vipera vya fasihi simulizi
              Wataalamu  mbalimbali  (kwa mfano Mulokozi na  Wamitila)  wamegawanya
              fasihi simulizi katika tanzu na vipera mbalimbali ambavyo vimeoneshwa katika
              Kielelezo namba 2.1.


                 6                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   6
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   6                     23/06/2024   17:54
   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22