Page 18 - Fasihi_Kisw_F5
P. 18

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                          Fasihi Simulizi





                 Hadithi           Semi              Ushairi        Sanaa za maonesho
          FOR ONLINE READING ONLY



                 Ngano           Methali            Nyimbo               Majigambo
                 Tarihi          Misemo             Mashairi              Tambiko
                Visasili         Mizungu            Ngonjera               Ngoma
                Vigano          Mafumbo             Maghani                Miviga

                 Soga          Vitendawili                               Vichekesho
                                                                          Ngomezi

                                                                            Utani
                                                                          Maigizo
                                                                     Michezo ya watoto

                             Kielelezo namba 2.1:  Tanzu na vipera vya fasihi simulizi

              Yafuatayo ni maelezo ya tanzu na vipera hivyo:

               Shughuli ya 2.2
              Kwa kutumia vyanzo mbalimbali  vya maarifa,  fafanua utanzu  wa hadithi  na
              vipera vyake.

              Hadithi
              Hadithi ni utungo unaotumia lugha ya mjazo (nathari) ili kueleza kisa fulani kwa
              mpangilio wa matukio. Mpangilio huo hutumia wahusika ambao ndio watendaji
              wa matukio hayo. Vilevile, hadithi huwa na kisa kinachofululiza tangu mwanzo
              hadi mwisho ili kukamilisha muundo wake.

              Hadithi huwasilishwa na msimuliaji mbele ya hadhira katika mandhari maalumu
              kama vile chini ya mti mkubwa, sebuleni, darasani au uwanjani. Vilevile, huweza
              kuwasilishwa kwa njia  za kidijiti. Aghalabu, simulizi  hufanyika  katika  muda
              maalumu, hususani baada ya kazi. Kama inavyoonekana katika Kielelezo namba
              2.1, utanzu wa hadithi  una vipera vitano  ambavyo ni ngano, tarihi,  visasili,
              vigano, na soga.






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            7
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   7                     23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   7
   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23