Page 11 - Fasihi_Kisw_F5
P. 11

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                                 Dibaji

              Kitabu hiki cha Fasihi ya Kiswahili: Kidato cha Tano kimeandikwa mahususi
              kwa mwanafunzi wa Kidato cha Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
              Kitabu hiki kimeandaliwa kulingana na Muhtasari wa Somo la Fasihi ya Kiswahili
          FOR ONLINE READING ONLY
              wa mwaka 2023 uliotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Baadhi
              ya maudhui ya kitabu hiki yamehamishwa kutoka katika Kitabu cha Kiswahili
              Shule za Sekondari Kidato cha Tano na Sita cha mwaka 2019. Kitabu hicho
              kiliandaliwa  kulingana  na  Muhtasari  wa Somo la  Kiswahili  wa mwaka  2009
              uliotolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

              Kitabu hiki kimegawanywa katika sura sita: Dhana na chimbuko la fasihi, Fasihi
              simulizi na fasihi andishi, Kutathmini kazi za kifasihi, Maadili katika fasihi,
              Ujumi katika kazi za kifasihi, na Kubuni kazi changamani za kifasihi. Maudhui
              ya kitabu hiki yamewasilishwa kwa njia ya matini, shughuli za kufanya, pamoja
              na vielelezo ambavyo vinachochea ujenzi wa umahiri unaokusudiwa kwa kila
              sura. Vilevile, katika kila sura kuna mazoezi yenye lengo la kupima na kujenga
              uelewa pamoja na ujuzi katika somo hili. Hivyo basi, mwanafunzi unapaswa
              kufanya mazoezi na shughuli zote zilizomo kwenye kitabu hiki pamoja na kazi
              nyingine utakazopewa na mwalimu. Pia, unapaswa kuandaa mkoba wa kazi kwa
              ajili ya kutunza kazi mbalimbali zinazotokana na ujifunzaji.

              Jifunze zaidi kupitia Maktaba Mtandao https://ol.tie.go.tz/videos













              Taasisi ya Elimu Tanzania


















                 x                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   10
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   10                    23/06/2024   17:54
   6   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16