Page 70 - Fasihi_Kisw_F5
P. 70

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Athari za sayansi na teknolojia katika maendeleo ya fasihi simulizi na
              fasihi andishi
              Maendeleo ya sayansi na teknolojia  yamesaidia  sana katika uwasilishaji na
              uenezaji wa fasihi simulizi. Maendeleo haya yamewezesha kuwapo kwa vyombo
              mbalimbali  vya uwasilishaji  kama  redio, runinga na simu. Redio na runinga
          FOR ONLINE READING ONLY
              zimekuwa na mchango mkubwa katika uwasilishaji na uenezaji wa kazi za fasihi
              simulizi. Kwa mfano, Redio Tanzania (kwa sasa TBC Taifa) imekuwa na vipindi
              ambavyo vimesaidia sana fasihi simulizi kuwafikia watu wengi. Kipindi kama
              vile  Mama  na Mwana  kilipendwa na watu wengi, hasa watoto, kwa sababu
              ya masimulizi  ya hadithi  mbalimbali.  Kipindi kingine ni  Cheichei  Shangazi
              ambacho kimekuwa na masimulizi ya hadithi, vitendawili na nyimbo. Baadaye,
              vilianzishwa  vituo  vingine  vya  redio  na  kuongeza  mawanda  ya  uwasilishaji
              na uenezaji wa kazi za fasihi simulizi. Kwa mfano, Redio One Stereo hurusha
              kipindi cha Watoto Wetu ambacho hupambwa na wimbo maarufu wa “Watoto
              Wasafi Moyoni”. Kipindi hiki hurushwa kila Jumamosi, ambapo watoto walioko
              studio na nyumbani huweza kushiriki katika uwasilishaji wa hadithi, methali,
              vitendawili, mafumbo na nyimbo.

              Pamoja na watoto kutoonana ana kwa ana, wanaweza kushiriki kwa njia ya
              kusikiliza.  Hivyo, hadithi ambazo  awali zilisimuliwa  kwa watu wachache,
              zinaweza kujulikana kwa wote wanaosikiliza. Mbali na vipindi vya watoto, redio
              zimekuwa zikirusha vipindi vingine vya fasihi simulizi. Baadhi ya vipindi hivyo
              ni Mkoa kwa Mkoa, Malenga Wetu, Ngoma Zetu, Zilipendwa, (TBC Taifa), Hizi
              Nazo (Redio One Stereo), Kwa Raha Zetu (Redio Clouds FM) na Mitikisiko ya
              Pwani (Times FM).

              Kwa upande wa runinga, uwasilishaji umekuwa tofauti kidogo. Katika runinga
              washiriki wana fursa ya kuona matendo yanayotendwa. Kuna vipindi vya watoto
              ambavyo huwasilisha kazi za fasihi simulizi. Mfano wa vipindi hivyo ni kipindi
              cha Watoto kilichoandaliwa na TET ambacho hurushwa na TBC1 na TBC2. Kipindi
              hiki kinachorushwa siku za Jumamosi na Jumapili, husimulia hadithi na michezo
              ya watoto. Pia, kuna kipindi cha Ubongo Kids (TBC1) ambacho kinahusu somo
              la hisabati na kusoma. Kipindi hiki huwa na matumizi ya nyimbo, usimulizi wa
              hadithi, na maigizo mbalimbali. Aidha, kituo cha ITV hurusha kipindi cha Watoto
              Show  ambacho hujumuisha nyimbo, ngoma,  methali,  vitendawili  na hadithi.
              Halikadhalika, runinga zimekuwa zikirusha vipindi kama vile, Mizengwe, Sanaa
              na Msanii, Mashamushamu ya Pwani na Hawavumi lakini Wamo (ITV). Vipindi
              vingine ni Futuhi, Bongo Beats na Msanii Wetu (Star TV). Aidha, kuna Fataki,
              Ngoma Zetu, Mchikicho wa Pwani Club Raha Leo Show (TBC1), na Mirindimo
              ya Pwani (Channel Ten). Vipindi vyote hivyo vimekuwa vikisaidia uwasilishaji
              na uenezaji wa fasihi simulizi.


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            59
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   59                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   59
   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75